Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Tuesday, July 31, 2012

PSG NA UTAWALA MPYA LIGI KUU UFARANSA


PSG: Sababu 5 za kwanini PSG wanapaswa kuogopwa na klabu nyingine za Ulaya kwa msimu ujao wa ligi

 

Uzoefu wa kocha Ancelloti

Carlo Ancelloti
Ni dhahiri kuwa msimu uliopita hakuwa mzuri kama ambavyo kocha Carlo Ancelloti angependa uwe.Akiichukua timu kutoka kwa mwalimu Antoine Kambouare,Ancelloti alikuwa na matokeo yafuatayo katika mechi zake 10 za mwanzo na PSG;5-5-0,kwa maana ya kushinda mechi 5,kutoka sare mechi 5 na kutopoteza mechi katika mechi 10 za mwanzo.Mechi 9 nyingine kwa klabu ya PSG katika ligi ya Ufaransa maarufu kama (Le Champione au French Ligue 1) zilikuwa kwa mfumo wa  6-1-2  kwa maana ya kushinda mechi 6,kutoka sare mechi 1 na kupoteza mechi 2.Tafsiri ya mechi zote hizo ni kuwa PSG walishindwa kushindana na timu ya Monperier ambayo baadaye ilitangazwa kuwa bingwa mpya wa Ligi kuu ya soka nchini Ufaransa.

Tukumbuke kuwa PSG pia walipoteza mechi dhidi ya mabingwa wa zamani wa Ligi hiyo klabu ya Olimpic Lyon.Ukichangaya na rekodi mbalimbali alizoweka akiwa na vilabu vya AC Milan na Chelsea, Hakuna shaka kuwa Ancelloti ataipa mafanikiwa klabu hiyo ya PSG kutokana na uzoefu wake katika michuano mikubwa na mechi za kimataifa hasa za Ligi ya mabingwa Ulaya ambapo mara ya mwisho PSG walishiriki ilikuwa ni mwaka 2003.

Kuwepo kwa wachezaji wazoefu.

Thiago Motta
Kama ilivyo kwa timu nyingine mbalimbali za Ulaya,PSG nayo imebarikiwa kuwa na wachezaji wazoefu ambao jukumu lao kubwa ni kuwaongoza wachezaji chipukizi.Mfano wa wachezaji hao ni Thiago Motta, Mohamed Sissoko, Maxwell, Diego Lugano na Alex.Pia ujio wa nyota wapya kama  Zlatan Ibrahimovic,Ezequel Lavezzi kutazidi kuimarisha timu hiyo.
Pia kuna kundi la wachezaji kama Sylvain Armand, Nene, Mathieu Bodmer, Zoumana Camara na  Nicholas Douchez ambao hawajacheza klabu kubwa zaidi ya PSG lakini wanauzoefu mkubwa na Ligi kuu ya Ufaransa na mchango wao mkubwa sana kwa PSG.

Wachezaji chipukizi

Mamadou Sakho
Wakati PSG wakijivunia kuwepo kwa wachezaji wakongwe,pia wanajivunia uwepo wa chipukizi wazuri kunako klabu hiyo. Na hapa bila shaka litakuja jina la Javier Pastore ingawa watu wanasahau kuwa kuna kundi kubwa sana la wachezaji chipukizi wenye uwezo mkubwa na ambao wana mchango mkubwa sana kwa klabu ya PSG.
Embu waangalie wachezaji chipukizi kama Jeremy Menez, Salvatore Sirigu, Kevin Gameiro, Blaise Matiudi na Mamadou Sakho wakiunda kundi la wachezaji nyota wenye matarajio na matumaini ya kufanya vyema kama wachezaji na timu yao ya PSG.Tukumbuke kuwa wachezaji hawa vijana wana uzoefu na mechi za kimataifa.




 

Usajiri mpya

 

Majina makubwa yataendelea kuja kunako klabu hii ya PSG kama walivyohaidi wamiliki wa timu hiyo kina Sheikh Makhtour wakiongozwa na mkurugenzi wa ufundi kunako klabu hiyo Leonardo.
Tayari wameshamchukua  Ezequiel Lavezzi toka (Napoli),Zlatan Ibrahimovic,Thiagi Silva toka (AC  Milan) pamoja Marco Verrati toka klabu iliyopanda daraja msimu h kunako ligi kuu ya soka nchini Italia maarufu kama Serie A.Usajiri wa Lavezzi na Ibrahimovic  utawahakikishia PSG kuwa na safu nzuri sana ya ushambuliaji ambao  watashirikiana na kina Kevin Gameiro pamoja na Anderson Nene.

 

Tatizo la klabu katika ushambuliaji lapata suluhu

Sehemu ya ushambuliaji msimu uliopita kunako klabu ya Paris Saint-German haikiuwa na makali sana kwani ilikosa kuwa na mwendelezo chanya kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa msimu na hivyo kuwagharimu PSG katika mbio zao za ubingwa wa Ligue 1.
Pamoja na kupata huduma za washambuliaji Kevin Gameiro na Guillaume Hoarau, PSG hawakupata mshambuliaji aliyekuwa na mwendelezo mzuri wa ufungaji magoli na hivyo kuifanya PSG kupoteza points nyingi sana katika Ligue 1.
Hivyo kuja kwa wachezaji Lavezzi na Ibrahimovic kutaimarisha nakuiongezea nguvu mpya safu ya ushambuliaji ya PSG kwa kuwa wachezaji hao wana uwezo mzuri pamoja na uzoefu mkubwa.


MAAJABU YA KIBIBI KIZEE KURUDI KATIKA UJANA


JUVENTUS-MAAJABU YA KIBIBI KIZEE KURUDI KATIKA UJANA



Andrea Pirlo
Ni miaka sita sasa tangu kutokea kwa ile kashfa kubwa ya upangaji matokeo iliyojulikana kama  Calciopoli ambapo dunia ilishuhudia kushushwa daraja kwa moja kati ya vilabu vikubwa  barani ulaya na duniani kwa ujumla timu ya Juventus.Ilikuwa ni miaka ya machungu kwa timu hiyo ya Turin hasa mashabiki wake ndani na nje ya Italia.Ila tangu wapande daraja msimu wa mwaka 2006-07, Juventus walikuwa katika wakati mgumu na mzito wa kuitengeneza timu yao mpaka msimu uliopita walipoutwaa ubingwa wa Escudetto(Serie A) wakiwapiku wapinzani wao AC Milan.
Ernesto Bronzetti
 Swaali; Je, Juventus wamerudi katika utawala wao kunako ligi ya Italia?
Mmoja wa mawakala wanaotambulika na FIFA Ernesto Bronzetti katika mahojiano yake na mtandao mmoja maarufu nchini Italia Tuttosport alisikika akitabiri kuwa Juventus wamerudi katika utawala wao kunako ligi ya Italia na haoni kama kuna timu za kuwazuia tena katika mbio zao za ubingwa msimu ujao.Bronzetti alitumia vigezo vifuatavyo katika kuthibitisha kauli yake.Namnukuu kwa maneno yake;
. “Juve are destined to dominate for the next few days,” Bronzetti told Tuttosport. “They have a stadium that is beginning to provide income, they put their hands on the best young players, and they have solid foundations, a great Coach and directors up to the task.” The way I see it, this side is even stronger than it was under Antonio Giraudo and Luciano Moggi.”Mwisho wa kunukuu.
Kwa ufupi wakala Bronzetti anazungumza kuwa Juventus wamejipanga kuanzia kwenye uongozi mpaka katika masuala ya ufundi uwanjani.Na hii inachagizwa na sera za sasa za klabu chini ya Rais Agnelli, uwanja wao mpya ambao waliutumia msimu uliopita katika ligi, na pia mshikamano wa mashabiki ambao kwa kipindi kirefu walivumilia shida za klabu mpaka sasa ambapo Juventus inaonekana kuanza kurudi katika zama zake za utawala katika soka la Italia.
Pia kwa kujifunza makosa ya viongozi waliopita nawazungumzia Alesio Seko,Giovanni Cobori Gigli Antonio Giraudo na wengineo,Juventus wameamua kutumia fedha kujenga kikosi chao lakini uwekezaji mkubwa ukifanywa katika kuwaibua vijana wenye vipaji na kuwapa nafasi ili waweze kuisaidia klabu hapo badaye.
Wengi wanakumbuka namna klabu ilivyowaacha bila kuwapa nafasi wachezaji vijana na wenye vipaji kama Sebastiani Giovinco na Antonio Nocerino kwenda vilabu vya Palermo na Parma na kuingiza majina makubwa ya kina Felipe Melo  pamoja na Diego na mwisho wa siku wachezaji hao kushindwa kuonesha makali na kupelekea kuuzwa na kupelekwa kwa mkopo katika vilabu vya Werder Bremen(Ujerumani) na Galatasary(Uturuki).Na hivyo uongozi wa sasa chini ya Rais Agnelli pamoja na mtendaji mkuu Marrota kuamua kufanya mseto wa wachezaji vijana pamoja na wakongwe.
Paul Pogba
Ni dhairi kuwa sasa Juventus wamepata timu mchanganyiko ambayo ina vijana wengi na ambao tunaamini wanaweza kuisaidia hapo baadaye.Tayari kuna vijana wenye vipaji kama Luca Marrone, Ouasim Bouy, Gabriel Appelt bila kusahau nyota wapya kama Richmond Boakye(Genoa), Paul Pogba(Man U),Kwawdo Asamoah(Udinese) na Nicola Leali.Uwepo wa wachezaji hao wakichanganyikana na wengine kama golikipa Gigi Buffon,Pirlo,Chierlin,Marchisio na Barzagli kutaipa Juventus uwezo mkubwa wa kupambana katika michuano mbalibali ndani na nje ya Italia.
MATARAJIO
 Ni kuiona Juventus ikija kwa kishindo kunako michuano mbalimbali kama mshindani makini na wa kweli katika Italian Serie A,Copa Di Italia na Klabu bingwa barani Ulaya hasa baada ya kuonekana dalili za kuanguka kwa vilabu vikongwe nchini Italia na jiji la Milan navizungumzia Inter na AC Milan.Hii inatokana na Juventus kuwa na miundo mbinu mizuri kama uwanja wake(Juventus Arena),benchi zuri la ufundi likiongozwa na kocha Antonio Conte bila kusahau nguvu pia ya kiuchumi pamoja na kuwa na kikosi kikubwa.

NI MSIMU MPYA KWA INTER MILAN


INTER MILAN NA MSIMU MPYA 2012-13

Claudio Ranieri
Hakuna shaka kuwa unapotaja jina la klabu ya Inter Milan unakuwa unataja moja kati ya vilabu bora na vikubwa barani ulaya sambamba na vilabu kama Manchester United,Barcelona,Real Madrid,Bayern Munich,Arsenal nk
Kilichotokea msimu uliopita wa Serie A kunako klabu hii kubwa duniani kiliwashangaza wengi mno kiasi cha kuanza kufikiria labda zile dhama za utawala wa Inter Milan nchini Italia,ulaya na duniani kwa ujumla zimeanza kupotea.Wengine wakasema kuwa bado jinamizi la aliyekuwa kocha wa timu hiyo kwa kipindi cha miaka 3 linazidi kuwaandama.Wengine nao hawakuwa nyuma kusema kuwa kurudi upya kwa klabu ya Juventus ndiko kumeitimisha shangwe za Inter Milan na wengine wanahusisha na kufanya vibaya kwa klabu hiyo na maamuzi yasiyokuwa na tija toka kwa Rais wa klabu hiyo Massimo Moratti pamoja na kurugenzi yake ya ufundi inayoundwa na Ernesto Paollilo pamoja na Marco Branca.
Haya yote yanakuja kutokana na kufanya vibaya kwa klabu hiyo ya Milan msimu uliopita wa (2011-12) katika Serie A kwani Inter Milan walishika nafasi ya 6 katika ligi hiyo maarufu barani ulaya.
Massimo Moratti
Rafael Benitez, Leonardo, Gian Piero Gasperini na Claudio Ranieri wote hawa kwa nafasi na muda wao walipita kunako klabu ya Inter Milan mara tu baada ya ya kuondoka kocha aliyeipa Inter mafanikio makubwa sana namzungumzia Jose Mourinho.Lakini makocha wote hao hawakuweza kurudisha zile nyakati nzuri kwa mashabiki wa Inter zilizodumu kwa takribani miaka 3 chini ya kocha Mourinho na mwisho wa siku kuambulia kufukuzwa na Rais wa klabu Massimo Moratti.

INTER YA MSIMU 2012-13 ITAKUWAJE?                                                     
Wachambuzi wa mpira wa miguu pamoja na mashabiki wa soka ulimwenguni wanajiuliza swali moja ya namna Inter itakavyokuwa msimu ujao wa ligi ya Serie A (2012-13) hasa baada ya kufanya vibaya msimu uliopita wa 2011-12.
Binafsi nategemea kuiona Inter yenye mabadiliko makubwa sana kuanzia nje ya uwanja kwa maana ya uongozi hasa katika maamuzi pamoja na ndani ya uwanja katika kufanya mabadiliko makubwa sana ya kiufundi na kimbinu.

MABADILIKO NJE YA UWANJA
Hapa moja kwa moja nazungumzia uongozi wa Inter Milan chini ya Rais wa klabu hiyo Massimo Moratti pamoja na kurugenzi yake ikiwa na Ernesto Paollilo pamoja,Marco Branca na Piero Ausilio.Hawa ni watu muhimu kwa mustakabali wa klabu  Inter kwa msimu unaokuja na hata kwa mafanikio ya klabu ya Inter hapo mbeleni.
Moja ya sababu ya kufanya vibaya kwa Inter msimu uliopita ni maamuzi yasiyokuwa na tija,macho wala maono yaliyofanywa na viongozi hao wa Inter Milan.Mfano ni kuuzwa kwa kiungo aliyetokea kuwa mhimili katika klabu hiyo namzungumzia Thiago Motta.Hakika kuuzwa kwa Motta tena dirisha dogo la usajiri mnamo mwezi januari kuriidhoofisha mno timu hiyo katika harakati za ubingwa wa Escudetto,Copa Di Italia pamoja ma michuano ya ulaya.
Wesley Sneidjer
Inter walionekana dhahiri kuwa na mapungufu sehemu ya kiungo pamoja na uwepo wa viungo shupavu kama Estaban Cambiasso na viungo wapya waliosajiriwa dirisha dogo mwezi huo huo wa januari mwaka huu 2012 nawazungumzia Fredy Guarin(Porto),Andrea Poli(Sampdoria),Angelo Palombo(Sampdoria) na wengine kama Ricky Alvarez,Dejan Stankovic na Wesley Sneidjer ambaye hakuwa msimu mzuri uliopita kwa sababu ya majeruhi na kufanya  idara hiyo ya kiungo kushindwa kuisaidia Inter kupata nafasi ya kushiriki michuano ya klabu bingwa ulaya mwakani ukiachilia mbali ubingwa wa Escudetto.
Tayari Rais wa klabu Massimo Moratti pamoja na ile bodi yake ya wakurugenzi ambayo kwa kiasi kikubwa imejaa ukoo wa Moratti kwa sababu Inter Milan ni timu inayomilikiwa na familia kwa muda mrefu sasa tangu enzi za baba Angelo Moratti ambaye amepewa heshima katika uwanja wa mazoezi wa Inter kuitwa jina lake ukifahamika kama Angelo Moratti Sports Centre.
Viongozi hao wameamua kutotumia sana fedha wakati huu kama ilivyokuwa kwa msimu uliopita ili kubana matumizi na kuhakikisha wachezaji vijana wanapewa  nafasi ya kucheza msimu ujao wa ligi na mashindano mengine kama Copa Di Italia.Uamuzi wa uongozi wa Inter ni kuhakikisha kuwa timu inajengwa upya na hasa wachezaji chipukizi wakipewa nafasi kunako kikosi cha Inter Milan.Na hiyo ndo sababu ya Rais wa klabu kuamua kumpa majukumu aliyekuwa kocha wa vijana wa klabu ya Inter Milan Andrea Stramaccioni ili kuweza kukisuka upya kikosi hicho cha Inter.

MABADILIKO NDANI YA UWANJA.
Tayari Inter wameshamsajiri mshambuliaji Rodrigo Palacios katika kujiimarisha ndani ya uwanja na kukiongezea nguvu kikosi kwani kuna hatihati ya kuondoka kwa baadhi ya nyota kama Giampaoro Pazzin, Maicon na Mauro Zarate kwenda kwa vilabu vya Juventus, Chelsea pamoja na Lazio.Tukumbuke kuwa tayari Diego Forlan ameshaondoka na kujiunga na klabu ya Internacional (Brazil) wakati kukiwa na wasiwasi kama kiungo mchezeshaji Wesley Sneidjer kama atabaki na klabu hiyo msimu ujao.
Rodrigo Palacios
Na dalili zinaonesha kuwa bado timu itaendela kusajili baadhi ya wachezaji na majina yao yakihusishwa na kuhamia klabu hiyo ya Lombard katika jiji la Milan.Majina hayo ni pamoja na Lucas Moura(Sao Paulo),Mattia Destro(Siena),Edinson Cavani(Napoli) na David Astori(Cagriali).
Kuondoka na kuwasili kwa baadhi ya wachezaji wakisajiliwa ama kurudi toka kwa mkopo kunako vilabu mbalimbali  katika  klabu hiyo ya Inter kama nyota chipukizi aliyekuwa ligi ya Hispania msimu uliopita akiichezea klabu ya Espanyol kunaweza kumfanya kocha  Andrea Stramaccioni kubadili mfumo uliozoeleka wa 4-3-1-2 au 4-3-3  na kuja na mfumo mpya kulingana na aina ya wachezaji waliopo Inter Milan.
Swali; Je tutegemee mfumo gani kwa Inter Milan msimu ujao?

NI MUDA WA VIJANA KUPEWA NAFASI
Mashabiki wengi wa soka duniani wanajiuliza kuwa wapo wapi wachezaji chipukizi kunako timu hiyo ya Inter Milan na mbona hawapewi nafasi?
Ukweli ni kuwa klabu ya Inter imejaliwa kuwa na wachezaji wengi vijana ambao wengine tayari wameshaanza kuonesha uwezo mkubwa katika timu hiyo.Wachezaji hao ni pamoja na Joel Obi,Luc Castaignoc, Marco Faraoni, Berretti, Alliezi Nazionali na Giovanissimi Nazionali, Lorenzo Crisetig na bila kumsahau mshambuliaji Samuele Longo.Hao wote kwa kiasi kikubwa inabidi wapewe nafasi taratibu ili kuzoea mafunzo ya mwalimu Stramaccioni pamoja na mifumo na falsafa ya mwalimu.
Javier Zaneti
Uwepo wa wachezaji vijana hao pamoja na nyota wengine kunako klabu hiyo kama Estaban Cambiasso,Javier Zaneti,Yuto Nagatomo,Fredy Guarin pamoja na wachezaji wapya kama Samir Handanovic,Rodrigo Palacios na nyota wengine watakaokuja kutaifanya klabu hiyo kuwa na kikosi kikubwa ambacho kitaleta ushindani kunako ligi ya Serie A.
Sitegemei makosa ya nyuma yatajirudia kwa Inter kuwauza nyota wake chipukizi pasipokuwatumia na kuona namna gani wanawezainufaisha klabu sasa na siku zijazo kama walivyofanya hapo nyuma kwa kuwauza Mario Balloteri na David Santon ambao binafsi nilitegemea wangekuwa na msaada mkubwa sana katika klabu hiyo hapo badae.
KILA LA KHERI INTER MILAN

MSIMU MPYA WA USAJIRI


Wapi atakuwepo Aquilan msimu ujao wa 2012-13?

Alberto Aquilan
Mnamo mwezi Machi mwaka 2003 katik jiji la Roma, kulikuwepo na tukio ambalo mashabiki wa moja kati ya vilabu vinazopatikana katika jiji la Roma naizungumzia klabu ya Associazione Sportiva Roma maarufu kama AS Roma hawatolisahau tukio husika.Ilikuwa ni mechi nzuri ya SERIE A ya msimu wa mwaka 2002/03 kati ya Roma vs Torino ambapo aliyekuwa kocha wa Roma kwa wakati huo namzungumzia Fabio Capello akifanya ujasili wa kumtambulisha kinda Alberto Aquilan.
Akiingia kucheza sambamba na Daniele De Rossi ambaye tayari alishawafunga Torino goli 1 katika mechi hiyo, Aquilan alionesha kipaji kilichomtabiria kuja kuwa moja kati ya mastaa wa badaye wa klabu hiyo ya Serie A pamoja na Ulaya kwa ujumla.
Akiwa na Roma,Aquilan amefanikiwa kutwaa mataji mbalimbali kama Supercopa Italiana mwaka 2006 na Copa Di Italia mwaka 2007.Mnamo mwaka 2009,aliyekuwa kocha wa Liverpool Rafael Benitez alimsajili Aquilan kwa hela za ulaya(EURO) MILION 17 kujiunga na Liverpool.
Lakini tangu aondoke katika jiji hilo takatifu la Roma, Aquilani anaelekea kusahaulika kunako medani ya soka.Hii inatokana na majeruhi ya mara kwa mara ambayo yamekuwa yakimwandama mchezaji huyo. Mshindi huyo wa Copa Di Italia mwaka 2007 na klabu ya Roma pamoja na ngao ya jamii maarufu nchini Italia kama SupercopaItaliana ameweza kucheza mechi 30 katika msimu mmoja tu kati ya misimu sita iliyopita akiwa na klabu za Liverpool na Ac Milan.
Na sasa ni msimu mpya wa Ligi mbalimbali za Ulaya unakaribia kuanza huku kuiwa na mashaka ya kuwa ni wapi mchezaji Alberto Aquilan atacheza msimu wa mwaka 2012-2013.
KILA LA KHERI AQUILAN