PSG: Sababu 5 za kwanini PSG wanapaswa kuogopwa na klabu nyingine za Ulaya kwa msimu ujao wa ligi
Uzoefu wa kocha Ancelloti
![]() |
Carlo Ancelloti |
Tukumbuke kuwa PSG pia walipoteza mechi dhidi ya mabingwa wa zamani wa Ligi hiyo klabu ya Olimpic Lyon.Ukichangaya na rekodi mbalimbali alizoweka akiwa na vilabu vya AC Milan na Chelsea, Hakuna shaka kuwa Ancelloti ataipa mafanikiwa klabu hiyo ya PSG kutokana na uzoefu wake katika michuano mikubwa na mechi za kimataifa hasa za Ligi ya mabingwa Ulaya ambapo mara ya mwisho PSG walishiriki ilikuwa ni mwaka 2003.
Kuwepo kwa wachezaji wazoefu.
![]() |
Thiago Motta |
Pia kuna kundi la wachezaji kama Sylvain Armand, Nene, Mathieu Bodmer, Zoumana Camara na Nicholas Douchez ambao hawajacheza klabu kubwa zaidi ya PSG lakini wanauzoefu mkubwa na Ligi kuu ya Ufaransa na mchango wao mkubwa sana kwa PSG.
Wachezaji chipukizi
![]() |
Mamadou Sakho |
Embu waangalie wachezaji chipukizi kama Jeremy Menez, Salvatore Sirigu, Kevin Gameiro, Blaise Matiudi na Mamadou Sakho wakiunda kundi la wachezaji nyota wenye matarajio na matumaini ya kufanya vyema kama wachezaji na timu yao ya PSG.Tukumbuke kuwa wachezaji hawa vijana wana uzoefu na mechi za kimataifa.
Usajiri mpya

Tayari wameshamchukua Ezequiel Lavezzi toka (Napoli),Zlatan Ibrahimovic,Thiagi Silva toka (AC Milan) pamoja Marco Verrati toka klabu iliyopanda daraja msimu h kunako ligi kuu ya soka nchini Italia maarufu kama Serie A.Usajiri wa Lavezzi na Ibrahimovic utawahakikishia PSG kuwa na safu nzuri sana ya ushambuliaji ambao watashirikiana na kina Kevin Gameiro pamoja na Anderson Nene.
Tatizo la klabu katika ushambuliaji lapata suluhu
Pamoja na kupata huduma za washambuliaji Kevin Gameiro na Guillaume Hoarau, PSG hawakupata mshambuliaji aliyekuwa na mwendelezo mzuri wa ufungaji magoli na hivyo kuifanya PSG kupoteza points nyingi sana katika Ligue 1.
Hivyo kuja kwa wachezaji Lavezzi na Ibrahimovic kutaimarisha nakuiongezea nguvu mpya safu ya ushambuliaji ya PSG kwa kuwa wachezaji hao wana uwezo mzuri pamoja na uzoefu mkubwa.
0 comments:
Post a Comment