Ni swali ambalo situ kila mpenzi
wa hizi timu mbili kubwa pale BUNDESLIGA linawaumiza kichwa bali pia wachambuzi wa soka kutoka kila pande
ya Dunia.Borussia Dortimund chini ya rais Dr Reinhard Rauball mkurugenzi mkuu Hans-Joachim Watzke, mkurugenzi
wa michezo na mchezaji mwenye lekodi ya michezo mingi Dortimund Michael Zorc kwa pamoja na Kocha Juggen Klopp a.k.a JK hakika wamefanya kazi kubwa sio tu
kuirudisha Dortimund katika makali yake bali pia kupata kile kinachoitwa kwa
sasa mpira Dortimund.
Dortimund wamepita
vipindi tofauti vya raha na karaha na tatizo kubwa likiwa katika usimamizi wa
fedha na kupelekea mpaka kufirisika na tishio kubwa likiwa lile la 2005.Westfallen
Stadion moja kati ya viwanja vikubwa Ujerumani na Ulaya ukikabidhiwa kwa
kampuni ya Insuarance ya Signal Iduna na uwanja kuitwa Signal Igunal Park mpaka
2016 ili kupunguza madeni ya Dortimund.
Unaikumbuka
Dortimund ya mwaka 1997 chini ya Ottmar Hitzfeld
ikiwa na nyota kama Karl Heinz Riedle kocha wa sasa wa Norwich Paul Lambert,kikosini
pia kukiwa na kinda aliyekuwa anakuja kwa kasi kweli Lars Ricken na sasa akisimamia timu ya vijana.Waliisasambua
Juventus 3-1 mbele ya Zinedine Zidane kuchukua Uefa Champions league na wakati
ule Intecontinetal cup wakiilaza Cruzeiro 2-0 hakika hii ilikuwa Dortimund
ambayo kurudia walichokifanya umekuwa ni mtihani kweli kweli.
JUGGEN KLOPP JK
Wamepita walimu wengi lakini yeye
ndo nembo ya ushindi sasa pale Westphalia.Achana na bajeti finyu ambayo hana
budi kwenda nayo huyu jamaa ameleta vitu viwili vikubwa kwanza ni mpira
Dortimund na nidhamu kubwa kikosini.Ametengeneza kitu ambacho walimu wengi kinawashinda kutengeneza kwamba
hakuna mchezaji mkubwa zaidi ya klabu.

Msimu uliofuta wengi wakiamini ule ulikuwa ni moto wea kifuu JK aliwashangaza tena akichukua makombe mawili kwa mara ya kwanza tena kwa kuweka rekodi ya kufikisha pointi 81 ni nyingi kuliko zote katika historia ya Bundesliga.Wakianza msimu bila ya mfungaji bora wa msimu uliopita Lucas Barios staili yake ya kuwajaza vijana kujiamini inamleta Lobert Lewandoski na kuwafanya mashabiki kumsahau kabisa Lucas Barios.
Kipindi cha majira ya joto wanamuuza
nyota Nuri Sahini kwenda Madrid lakini anamuinua Shinji kagawa kuziba pengo
mashabiki wanamsahau Sahin.Msimu huu wanamuuza Shinji kagawa kwenda Manchester
United wanamrudisha nyota wao waliyemlea na kumkuza wenyewe kutoka Gladbach
Marco Reus kuziba pengo la kagawa na nina uhakika watu watamsahau Shinji
Kagawa.
Swali kubwa ni je Dortimund ataendelea
kuitambia Bayern Munchen na Bundesliga kwa ujumla? Hebu tuone misimu huu utakovyokuwa.
MSIMU HUU UNAONEKANA MGUMU
MSIMU HUU UNAONEKANA MGUMU

USAJILI
Baada ya kumkosa Marco Reus Bayern wamemsajili Xherdan Shaqili pembeni kule kwa Roben ambaye sio tu kwamaba ana historia mbaya ya majeraha lakini pia akionekana kuigharimu Bayern kwenye matukio muhimu lakini kubwa abisa ambalo hata vyombo vingi vya habari vya Ujerumani vilikuwa vikimpigia kelele ni la kuwa mmbinafsi uwanjani.Lakini pia Wamewasajili Claudio Pizzaro na Mario Mandzukic kwenye ushambuliaji.Wengi watajiuliza kwa nini Claudio Pizzaro na Mario Mandzukic na tayari Bayern wana mtu hatari mbele Mario Gomez? Lakini amini usiamini pamoja na kupitwa na Messi na Ronaldo pekee kwenye kufumania nyavu Ulaya msimu uliopita Gomez amekuwa akipondwa sana na wakongwe wa Bayern Munchen na hata rais wa Bayern Ruminage akidaiwa kupoteza nafasi nyingi sana na kufunga chache.
Dortimund kwa upande wake Baada ya
kuondokewa na Kagawa walimsajili Marco Reus. Ni mtu hatari sana aking’ara na
Gladbach msimu uliopita na wakuwafanya msimu huu washiriki klabu bingwa barani
ulaya.Anatazamiwa kutengeneza uwiano na uelewano mzuri na kinda mwenye kipaji
cha hali ya juu ujerumani kwa sasa na rafiki yake toka timu ya vijana
ya Dortimund Mario Gotze. Ujio wa Gotze ni kama usajili mpya kwani kwa kipindi kirefu amekuwa akiandamwa na majeraha na hakika wananifanya niisubri Bundesliga kwa hamu sana.Lakini pia
wamewasajli Leonardo Bittencourt,Julian Schieber na Olivier Kirch.Ujio wa Kirch
Unatazamiwa kutoa msaada pembeni kule
beki ya kulia kwa Lukasz Pisczcek ambaye majeraha kidogo yamekuwa ya kimsumbua.
UZOEFU WA MICHUANO MIKUBWA
Tatizo kubwa ambalo laweza kuisumbua
Dortimund msimu huu ni michuano ya Virabu bingwa barani Ulaya.Japo walicheza
vizuri katika makundi msimu uliopita lakini kimbinu na kiakili Dortimund
walionekana hawajakomaa na hata kocha Juggen Kopp akisema michuano hii imekuwa
mikubwa sana kwa baadhi ya nyota wake.Japo walianza vibaya ligi lakini kushika
nafasi ya mwisho kwenye kundi lake lililokuwa na Arsenal,Marsille na olimpiacos
iliwafanya wachukue Bundesliga bila kupoteza hata mchezo mmoja katika yote
iliyokua imebaki baada ya kuutoa mzigo wa klabu bingwa.
Dortmund must find a way to recover the gap left by Shinji kagawa, Reus hmslf cnt, nor Mario Gotze who seems 2 be addicted wit injuries, jus like tom cleverley and jack wilshare. .shinji was such important player in their squard, made them succed wot they've succeeded. .
ReplyDelete