Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Wednesday, August 1, 2012

KUTOKA NELSON VIVAS MPAKA ROBIN VAN PERSIE NI MISIMU SABA SASA ARSENAL BILA KOMBE




N
akumbuka wakati Fulani nipo chuoni pale chimwaga jengo Fulani maarufu wanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma wanalifahamu sana baadhi ya vipindi au[ lectures] na mihadhara mbalimbali inafanyika pale kuna kozi flani hivi kila ikiisha wanafunzi wanahisi kuchanganyikiwa.
 Nikamuuliza mwalimu wangu wa somo hilo akaniambia  usishangae sana ukiona kuna kitu nimekufundisha  halafu ukahisi kama unakaribia kuchanganyikiwa hivi ujue unakaribia kuelewa kwasababu wakati wa kuchanganyikiwa ndo wakati wa ubongo kuchambua kipi cha kuelewa na kufuata na kipi sio kitu cha msingi na kuachana nacho.

Nao wahenga wana msemo wao wanasema ukijua tatizo  ujue unakaribia kulipatia jawabu  ndo kitu kinakaribia kutokea pale kwenye viwanja vya London Colney na Emirates kwa pamoja.

Ukitua uwanja wa Emirates leo kitu unachokutana nacho mara moja ni sanamu za watu watatu huyu ni Arsene wenger kocha anayetajwa kuwa ndo mwalimu mwenye mafanikio kuliko wote pale Arsenal na mchango wake kwenye soka la Uingereza haupingiki,akifuatwa na mfaransa mwenzake mfumania nyavu bora wa Arsenal na ligi kuu pale Uingereza Thiery henry pembeni kidogo  ni Toni Adams moja kati ya mabeki wakati bora kabisa pale Arsenal na England.

Hizi ni nembo za ushindi na ushujaa pale Emirates na kwa pamoja huu ni utambulisho kwa mashabiki, makinda wanaochipukia pamoja na wachezaji wapya wanaosajiliwa kujionea moja kati ya vitu vizuri vilivyowahi kutokea katika historia ya timu yao.Ukienda popote vilabu vyenye mafanikio makubwa katika soka watu hawa wana nafasi kubwa sana  lakini si Arsenal ukija hapo mambo ni tofauti kidogo hapa utaishia kuambulia mikanda ya video na simulizi tu hakika ukiwa kama mpenzi wa hii timu hakika nilazima utahisi kuchanganyikiwa.

Hapa majuzi dirisha dogo la mwezi January tulimshuhudia Thiery henry akirudi Arsenal na ukiacha Van persie huyu jamaa ni miongoni mwa watu waliochangia kwa kiasi kikubwa Arsenal kugeuza msimamo waligi ya  premier pale Uingereza kuitoa Arsenal katika kile kinachoaminnika ni kuanza msimu vibaya ambako hakujawahi kushuhudiwa katika historia ya timu hiyo.Huyu alikuwa mtu muhimu sana pale eamirates  ukitoa mzee Wenger, kuanzia London Colney mpaka kwenye vyumba vya kubadilihia nguo,hata wale wachezaji makinda ambao walipata kumuona kupitia luninga zao ama kwenya mikanda ya video hakika iliwaongezea kitu cha ziada.

Hakika anayewza kurishuhudia kwa uzuri kabisa  ni kinda mwenye kipaji cha hali ya Chamberlain anasema” nilipomwona kwa mara ya kwanza nilimshangaa sana nilimuona kama si mchezji kama mimi lakini baada ya kufanya naye mazoezi ndo nikahisi naye mtu”wakati wa mechi na Manchester pale Emirates akasema “wakati tunakimbia naye aliniambia uwezo wangu na amesesma vitu ambavyo naweza kufanya na akanisisitiza niendelee kufanya hivyo.Hivi ndo vitu ambavyo vinaweza kumtofautisha Benick Afobe na Dan Welback ambaye kila siku anafanya mazoezi na watu ambao wamefanya vitu vikubwa na klabu kama kina Ryan Giggs na Paul Scholes sasa Henry  yupo zake marekani lazima uhisi kuna kuchanganyikiwa kama kweli una mapenzi na timu yako.

Nakumbuka wakati ule kuelekea msimu  mpya miaka nane sasa imeepita Arsenal wakianza msimu kama mabingwa watetezi ni kipindi cha kuwaongezea  mikataba Thiery henry,Patric Vieira na Denis Bergkamp huku mikataba yao ikiwa imebaki miaka mitatu na mchezaji pekee anayeuzwa ni Nelson Vivas kama ni leo timu ikiwa Uchina ikijindaa na msimu mpya ungesikia taarifaa za  kuuzwa kwa Sebastiani Squilacci, Maroune Chmakh na imeshaandaa mikataba minono kwa kina Fabregas,Nasri,Walcott pamoja na Vanpersie lakini siku hizi mambo yamebadilika sana wanaotakiwa kubaki ndo wanaondoka wanaotakiwa kuondoka ndo wanabaki katika mazingira haya kama una moyo wenye nyama kama wangu lazima uhisi kuna kuchanganyikiwa.

Arsene wenger na Arsenal wanammisi sana mtu anayeitwa Devid Dein huyu alikuiwa ni zaidi ya makamu mwaenyekiti alikuwa  yuko kwaajili ya kumfanya kila mtu sio tu anafanya kazi bali pia kuifurahia na kuifanya Arsenal pahala pazuri kila mtu angetamani kuishi.Sasa mtu huyu ameondoka na kila kitu pale  kuanzia makombe mpaka mastaa wa timu Van persie ndo anamalizikia katika kile kizazi ambacho kilipokea tuzo ya kuwa timu bora kuwahi kutokea katika kipindi cha miaka ishirini ya uhai wa Bacrays English Premier League.

Kitu pekee alichobakiziwa ni mpira Wenger na ndo hi ndo jeuri pekee ya mashabiki  kwenye vibanda vya kuangalizia mpira pale Shimo la udongo  jamaa achilia mbali kwamba ndo aliyempa shavu wenger akimtoa Japan huko vichakani Nagoya Grumpus 8 lakini pia ndiye aliyekuwa msaada mkubwa katika kuwaleta nyota kibao Emirates kina Denis,Thiery henry alikuwa ni kama Pini Zahavi wa Arsensal manake alikuwa anazijua fitina kwelikweli.

Huyu jamaa alikuwa ni zaidi ya kiongozi zaidi ya miaka 20 kunzia London Colney mapaka kwenye vyumba vya kubadilishia nguo angefurahi na kulia na mashabiki pale Old Trafford kwenye kile kipigo cha 8-2 toka kwa mashetani wekundu. Leo kuna kundi la wafanya biashara kundi la wachuuzi wamarekani hawa kina Stan Kroenke hawa unachowaza ndugu yangu Mayenje sio wao wanachowaza wapo kimfuko zaidi kifaida furaha yako sio furaha yao wakati wewe ukilia msimu wa saba hujashanglia kombe wao wako visiwa vya Berbados wanafungua shampeini lazima utahisi kuchanganyikiwa ila kwa mujibu wa mwalimu wangu mambo ndo yanakaribia kukaa vizuri.

 Ukimuona mzee wenger katikati ya pambano pale Wembley anasimama anakaa kama kuna mtu anamchezesha hivi anakunywa maji anatema anatupa chupa yenyewe kabisa kachanganyikiwa  na unaweza kusema ni mtu wa jabu sana au ndo yale ya kuficha mchele mpaka siku ya krismas au IDD huku watu wanakufa njaa manake jinsi ya kumaliza miviga.

 Anajua manake ameshaozesha watoto na ana wajukuuu,achana na sera na mvurugano uliopo kati ya watu wawili wanaohodhi hisa nyingi Stan Kroenke pamoja na Ulshar Usmanov unamuacha vipi Dennis Bergkamp ajiunge na Ajax au Patrick Viera ajiunge kama mkrugenzi wa maendeleo ya michezo huku ukiwahitaji kwa kiasi kikubwa ,fikiria kueleke mchezo Fulani wa ligi na labda Manchester city pale uwanja wa Ethadi huku Fabregas akiwa na mawazo kuelekea mchezo huo akicheki pembeni kuna Patrick Viera akitabasamu nakumuelezea jinsi walivyompiga City nje ndani katika ule msimu anamaliza vita kama ilivyoanza ni msimu ambao Arsenal wanamaliza wakiwa hwajapoteza mchezo wowote sio Highbury wala Oldtraford.
Kuna wakati Fabregas mahesabu yalikuwa hayaendi kabisa kama kachanganyikiwa hivi anatamani kumwambia kitu mzee Wennger anashindwa akicheki pembeni anamwona Craig Eastmond na Watt Sanchez juu kabisa hapo anakutana na lile kundi la machinga kutoka marekani wao lillowaleta mjini ndo haswa wanalifanya kwa asilimia mia moja unachowaza ndugu yangu shimo la Udongo pale sio wao wanachowaza lazima uhisi kama unachanganyikiwa hivi.

Fabregas kwake  ni kama kukabidhiwa jezi huku akiwa mchezo hujaulewa alipewa jukumu la kuwa baba wakati na yeye alikuwa mtoto aliyehitaji kulelewa alitamani sana lile somo la ziada ambalo Messi,Iniesta,Xavi wanalipata toka kwa akina Guardiola mwisho unajua alisema nini “wewe ni mtu muhimu sana katika maisha yangu akitoka baba yangu aliyelala na mama yangu nikazaliwa mimi wewe ndo unafuata” lakini sina budi kusema usiku mwema kama ambavyo Van persie anamwambia leo lazima uhisi kunyanganyikiwa kama kweli una mapenzi ya ukweli na timu yako.

Arsenal ni moja kati ya vijiji ambavyo havina wazee na ndio maana mpaka sasa ni msimu wa saba sasa Wanacheza soka ambalo imekuwa ndo kielelezo cha soka bora ulimwenguni kwa sasa lakini bado hawajaonja vikombe na wameishia kuskia nderemo,vifijo na  na vigelegele kwenye kijiji cha wenzao hapohapo kaskazini mwa LONDON yani Chelsea.

Wako wapi kina Toni Adams,yuko wapi Yule mwanaume wa shoka aliyekuwa tayari kuitumikia Arsenal bila hata senti  pale katikati ya dimba kumpa somo la ziada ndugu yangu Abou Diaby jinsi ya kupata pointi tatu muhimu hata pale inapoonekana zingepotea,yuko wapi Sol Campbell ammpe somo la ziada Laurent Cocilienly anapolala siku ya mviga pale Wimbley,wapi Dennis Bergkapm ampe Vanpersie somo la ziada kwamba sio kila mahali atakuta nyasi za kijani sio kila mahali watamuimba “he scores when he wants”  kama ilivyo sasa kwenye mitaa na barabara za Brayantwoods,Gillesple hakika ukiyawaza haya lazima uhisi unachanganyikiwa.

Ujenzi wa moja kati ya viwanja vizuri  Ulaya uliogharimu takribani pauni za kiingereza million 500 ni kati ya vitu Wenger anapigiwa upatu kuwa nyuma ya mafanikio yake.Malengo ya kujenga  uwanja ni yale yale kuendelea kuifanya Arsenal kuwa moja kati ya timu kubwa Ulaya.

 Na kitu pekee ambacho kimeiangusha mpaka sasa ni jinsi ya kulipa deni la uwanja na kuendelea kulinda heshima yake kama timu kubwa pale Uingereza na Ulaya kwa ujumla.Njia walizochagua ni pamoja na kutegemea mapato ya ndani ikiwa ni pamoja na kupandisha tiketi za kuingilia uwanjani na kupunguza mishahara ya wachezaji  ambacho kinamuondoa Van Persie japo anajaribu kukanusha vikali.

 Msimu huu tiketi zinonekana kupunguzwa kwa kiasi kikubwa hasa kwa mechi za nyumbani pamoja na kuuzwa kwa wachezaj nyota na kununua wale wa bei rahisi washindane na timu ambazo zina mashuga dady kama vile Chelsea pamoja na Manchester city hakika ukiyawaza haya lazima uhisi kuchanganyikiwa kama kweli ni shabiki wa ukweli.

Japo Arsenal imekuwa ikishuhudia kuondokewa na nyota wake miaka ya hivi karibuni. Kwa mfano 2007 Thiery henry, 2008 Hleb na Flamini,2009 Adebayor na Kolo Toure,2010 Eduerdo,2011 Fabregas na Nasri,2012 Van persie naye ameshatangaza kutoongeza mkataba.Arsenal imeonekana kutoathirika sana. Mathalani msimu uliopita ikimaliza nafasi moja juu ya wakati wa Fabregas na Nasri.Hata Thiery hivi karibuni anasema nanukuu “ kama shabiki wa Arsenal ningependa kuona VanPersie anabaki lakini hata kama akiondoka Arsenal itaendelea kuwa imara”.Anaendelea wakati ule mimi nilipooondoka kila mtu alilia lakini baada ya hapo Arsenal ilimaliza poits nane zaidi ya msimu niliokuwepo.

Japo ndani ya misimu saba sasa hawajachukua kikombe chochote lakini bado imeendelea kulinda hadhi yake ulaya ikifuzu mala 16 ni nyingi zaidi kuliko pengine kuliko timu yoyote ya premier na chini ya Wenger haionekani kutofanya hivyo hivi karibuni na zaidi kukaribia kabisa zile siku ambazo Vanpersie na mashabiki wanazitoa.

0 comments:

Post a Comment