Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Tuesday, July 31, 2012

MSIMU MPYA WA USAJIRI


Wapi atakuwepo Aquilan msimu ujao wa 2012-13?

Alberto Aquilan
Mnamo mwezi Machi mwaka 2003 katik jiji la Roma, kulikuwepo na tukio ambalo mashabiki wa moja kati ya vilabu vinazopatikana katika jiji la Roma naizungumzia klabu ya Associazione Sportiva Roma maarufu kama AS Roma hawatolisahau tukio husika.Ilikuwa ni mechi nzuri ya SERIE A ya msimu wa mwaka 2002/03 kati ya Roma vs Torino ambapo aliyekuwa kocha wa Roma kwa wakati huo namzungumzia Fabio Capello akifanya ujasili wa kumtambulisha kinda Alberto Aquilan.
Akiingia kucheza sambamba na Daniele De Rossi ambaye tayari alishawafunga Torino goli 1 katika mechi hiyo, Aquilan alionesha kipaji kilichomtabiria kuja kuwa moja kati ya mastaa wa badaye wa klabu hiyo ya Serie A pamoja na Ulaya kwa ujumla.
Akiwa na Roma,Aquilan amefanikiwa kutwaa mataji mbalimbali kama Supercopa Italiana mwaka 2006 na Copa Di Italia mwaka 2007.Mnamo mwaka 2009,aliyekuwa kocha wa Liverpool Rafael Benitez alimsajili Aquilan kwa hela za ulaya(EURO) MILION 17 kujiunga na Liverpool.
Lakini tangu aondoke katika jiji hilo takatifu la Roma, Aquilani anaelekea kusahaulika kunako medani ya soka.Hii inatokana na majeruhi ya mara kwa mara ambayo yamekuwa yakimwandama mchezaji huyo. Mshindi huyo wa Copa Di Italia mwaka 2007 na klabu ya Roma pamoja na ngao ya jamii maarufu nchini Italia kama SupercopaItaliana ameweza kucheza mechi 30 katika msimu mmoja tu kati ya misimu sita iliyopita akiwa na klabu za Liverpool na Ac Milan.
Na sasa ni msimu mpya wa Ligi mbalimbali za Ulaya unakaribia kuanza huku kuiwa na mashaka ya kuwa ni wapi mchezaji Alberto Aquilan atacheza msimu wa mwaka 2012-2013.
KILA LA KHERI AQUILAN

0 comments:

Post a Comment