SUPERCOPA NI NINI?
Supercpopa ni mechi inayowakutanisaha bingwa wa ligi kuu
nchini Hispania maarufu kama La Liga na bingwa wa kombe la mfalme kila mwezi wa
nane kila mwaka.Msimu wa 2011-2012 mechi kama hii ilichezwa wakati huo Fc
Barcelona alikuwa bingwa wa La Liga na Real Madrid alikuwa ndio bingwa wa kombe
la mfalme na matokeo Barcelona ilichukua kombe kwa jumla ya magoli 5-4,
wakitoka 2-2 Bernabeu na Nou Camp
wakatoka 3-2 Berbabeu.Safari hii
Rea Madrid akishinda La Liga na Barcelona akichukua kombe la mfalme na ngoma ikianzia Nou Camp na baadae Bernabeu je
ni zamu ya Mourinho?
Mpambano huu kila siku unaongezeka msisimko na mpaka imefika
hatua watu wakaupa jina la mechi ndani ya mechi ndio unashangaa? Ndani ya mechi
moja kuna mechi nyingine zina endeleam kwa mfano
MOURINHO vs VILANOVA.
Je hii sio mechi? Mwezi wa nane mwaka jana mechi ilikuwa na
vurugu nyingi sana japo iliisha kwa Mourinho kupoteza pambano lakini pia
akimtia Vilanova vidole vya macho wakati huo akiwa kama kocha msaidizi wa
aliyekuwa kocha wa Barcelona wakati huo Pep Guardiola.
MOURINHO.
Kutoka the’ Special one’ mpaka sasa akjiita the’ Only one’
huyu jamaa haishi vituko.Anajiita hivi kwa maana kwamba ameshaziteka ligi zote
kubwa Ulaya unakataa nini? Ebu cheki
hizi takwimu akichukua makombe 17 na vilabu vitatu tofauti sio the Only One? Alinza na Fc Porto alichukua ligi mara 2,Portugal cup 1 na
champions league 1 na Supercopa1 hapo ni Ureno. Uingereza kazi na Chelsea ligi
2 FA cup 1 kombe la ligi(Carlinmg Cup) 2 na Ngao ya hisani( Community Shield)
1. ITALY. Hapa kazi inafanyika na Inter Milan, alinza na Sirie A 2 (scudetti)
Copa Italia 1,Champions league1 na Supercpoa 1 hakika ni yeye pekee.
Mourunho ni mtu anayependa kucheza mind game na tayari
ameshasema Superopa kwake sio muhimu na kama angeambiwa achague basi angechagua
kilichotokea msimu uliopita apoteze Supercpoa lakini ashinde ligi je ni kweli?
Ebu cheki hizi takwimu.Supertaka C.de Oliveira (Porto 2003) Community
Shield (Chelsea 2005)Supercopa Italina
(Inter Milan 2008. Ukizingatia kwamba Mourinho ameshashinda La liga pamoja na
kombe la mfale ni dhahiri washahiri anaihitaji Supercpoa kwenye CV yake na
baada ya” the special one” na the” Only One” nanai anayejua baada ya kulipata
atajiita nani?
VILANOVA.
Ameshudia Barcelona ikichukua vikombe vingi chini ya Guardiola
na yeye akiwa ni msaidizi tu sasa ni nafasi yake kupata kombe lake la kwanza
akiwa kama kocha mkuu.Anaonekana ni mtu makini na ndio maana Barcelona
wakamchagua kuwa kama kocha mkuu japo anaonekana mtu mwenye presha sana hasa
labda ni kutoka na kivuli cha mafaniko ya Guardiola.Vilonova anataka
kuwaonyesha watu Barcelona baada ya Guardiola maisha baada ya Guardiola kwmba
yanawezekana.
MESSI vs RONALDO
Wachezaji bora kabisa duniani kwa sasa na tayari kuna
maswali kwamba tayari wawepo kwenye orodha ya magwiji kama kina Pele ,Maradona
na wengine wengi ndio unashangaa nini? Na wakati Dunia na pande za kuu nne wamezipunguza na kuzifanya mbili? Huku kuna
wafuasi wa MESSI na huku kuna wafuasi wa RONALDO. Na miaka 4 sasa iwe ni
mchezaji wa FIFA ama UEFA
ni hao wawili ndo hupigiwa kula za mwisho japo Messi ameitetea nafasi ya
kwanza mara kadhaa.
KIUFUNDI.
Barcelona au Baugrana ni walewale japo kocha sio Pep
Guardiola ila mbinu zao na imani ya mifumo yao ni ile ille tunasema chupa tu
ndio mpya mvinyo ni ule ule.Mechi hii mara nyingi hutumika kutambulisha
wachezaji wapya kwa hiyo kitu pekee tunachotegemea ni kucheza kwa Alex
Song.Barcelona ni ile ile kama tulivyoizoea mfumo wao ukionekana 4-3-3 kwenye
makaratasi lakini kitendaji unabadilika na kuwa 3-4-3 kama tulivyoona mechi na
Manchester na pia wikiendi walpocheza na Real Sociedad. Messi anaonekana yupo
tayari kiakili hasa baada ya kufunga mawili
katika ushindi wa 5-1 kwenye La liga na pia tunategea Davi Villa
atampunguzia Messi zile 44% za ufungaji
wa magoli msimu uliopita baada ya kurudi kutoka miezi 8 ya majeraha.
Huku Loss Blacos ama Real Madrid nao wanaonekana ni wale
wale hasa kutokana na ukweli kwamba hawajafanya usajili japo tunategemea Luka
Modric kujiunga nao hivi karibuni. Achilia mbali majeruhi ya mtu kama pepe pia
wanaweza wakawapoteza Ricardo Carvaryo na Nuri Sahini ambaye anaelekea Arsenal
kwa hiyo tunategemea Raul Arbiol pamoja na Ramos. Mfumo wao wa 4-2-3-1
unaonekana kuendelea kutumika Alonso na Khedira kwenye 2, Ronaldo,Ozil na
Dimaria kwenye 3, na Benzema ama Higuain kwenye 1.Sare ya 1-1 na Valencia
wanapaswa kushangilia kwani hawakuistahili wakicheza hovyo kabisa sijui kwamba homa ya El Clasico
ilikuwa imeshaingia ila nawategemea kubadilka sana maana hii ni biashara
nyingine kabisa.
JE UNAJUA?
Pique vs Ronaldo |
Je unajua kwamba Real Madrid na Barcelona wameshakutana
tayari mara 220, Real Madrid akishinda mara 87 na Barcelona akishinda mara 86
wakienda sare michezo 47.
Je unajua kwamba Barcelona wamepoteza mchezo mmoja tu katika
jumla ya michezo 8 waliyocheza hivi karibuni na Real Madrid? Barcelona
wameshinda mara 4 na sare 3.
Je unajua Barcelona ameshinda fainali zote tatu mfululizo za
Supecopa zilizopita? 2009 alishinda dhidi ya Athletic Bilbao, 2010
alishinda dhidi ya Sevilla na 2011
akiwafunga Real Madrid.
Je Unajua kwamba Lionel Messi ameshafunga magoili 13 katika
El Clasico 19 zote alizocheza? Anapitwa goli 1 na gwiji la Real Madrid Cesar Rodriguez mwenye magoli 14.
Je unajua Real Madird chini ya Mourinho katika safari nne
walizoenda Nou Camp wamepoteza mchezo mmoja tu? Wameshinda 1 na sare 2.
Je unaijua Rekodi ya Mourinho kwenye El Clasico? Ameshinda 2
sare 4 na amefungwa 5.
Je unajua kwamba kadi nyekundu 8 kati ya 10 zilizotolewa
kwenye El Clasico zimeenda kwa wachezaji wa Real Madrid?
Je unajua kwamba Christiano Ronaldo amefunga magoli 6 tu
katika mechi zote ambazo amekutana na Barcelona? Hii injumuisha mechi
alizocheza pia wakati akiwa na
Manchester Utd
0 comments:
Post a Comment