Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Saturday, January 26, 2013

YANGA KUANZA KIBARUA KESHO LIGI KUU VODACOM

 
Young Africans Sports Club Mabingwa wa Kombe la Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kagame Cup) kesho inatarajiwa kushuka dimbani kucheza mchezo wake wa kwanza wa ufunguzi wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom dhidi ya timu ya Tanzania Prisons kutoka Mbeya mechi itakayoanza majira ya saa 10 jioni katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es saalaam.
 
Mara baada ya kuweka kambi ya takribani wiki mbili katika mji wa Antalya nchini Uturuki kikosi cha Young Africans kimerejea kikiwa na morali ya hali ya juu, wachezaji na benchi la ufundi wakihitaji kushinda kila mchezo unaowakabli ili kujiweka katika hali nzuri ya kutwaa Ubingwa wa Vodacom.
 
Katik micheoz miwili ya kujipima nguvu  kabla ya kuanza kwa duru la pili la ligi kuu Young Africans ilishinda michezo yote, mchezo wa kwanza kwa mabao 3-2 dhidi ya timu ya Black Leopard kutoka nchini Afrika Kusini kabla ya kushinda tena 2-1 katika mchezo wa marudiano dhidi ya timu hiyo ya Afrika Kusini katika mchezo uliofanyika jijini Mwaza. 
 
Young Africans ambayo inaongoza msimamo wa ligi kuu ya Vodacom kwa kuwa na alama 29 alama tano zaidi ya timu inayoshika nafasi ya pili ikiwa na alama 24, huku ikiwa imefunga jumla ya mabao 25 na kufungwa mabao 10 tu katika mzunguko wa kwanza wa ligi kuu ya Vodacom
 
Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza uliochezwa katika dimba la uwanja wa Sokoine jijini Mbeya timu zilitoka sare ya bila kufungana mchezo ambao pia ulikuwa ni wa waufunguzi  katika araundi ya kwanza.
 
Kocha Mkuu Ernest Brandts amesema kikosi chake kimekamilika, kiakili, kiafya na kimorali hivyo anaamini vijana wake wataibuka na ushindi katika mchezo wa kesho dhidi ya Prisons kutoka Mbeya.
 
Kikosi cha wachezaji 27 leo kimefanya mazoezi yake ya mwisho leo asubuhi katika uwnja wa mabatini kijitonyama huku wachezaji wote wakiwa katika hali nzuri ya kimchezo na hakuna mchezaji majeruhi hata mmoja. 
 
Timu imeingia kambini leo asubuhi katika hostel zilizopo makao makuu ya klabu makutano ya mitaa ya Twiga/Jangwani.

0 comments:

Post a Comment