Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Friday, January 4, 2013

SPORTS GALLA


 
Jason Nono Mayele yaweza kuwa jina geni kidogo kwa watu wengi hasa wapenzi wa soka na wale wasio wa soka.Huyu ni mchezaji wa zamani wa vilabu vya La Berrichonne de Châteauroux au Châteauroux) za nchini Ufaransa pia amewahi kuvichezea vilabu vya Cagliari  pamoja na Chievo Verona za nchini Italia.Ameshawahi  pia kuichezea timu ya taifa ya Congo DRC katika miaka ya 2000 mpaka 2002.

Jason Nono Mayele alizaliwa mnamo tarehe ya 4 Januari 1976 pale Kinshasa nchini DRC Congo.Akicheza katika nafasi ya winga/mshambuliaji,Jason alianza maisha ya soka katika klabu ya Brunoy FC ya nchini Ufaransa kabla ya kuhamia klabu ya Chateauroux na kisha kwenda klabu ya Cagliari kabla ya kumalizia soka lake kunako klabu ya Chievo Veron ambapo ndipo mauti yalipomkuta.

KIFO CHAKE.
Kifo cha Jason Nono Mayele kilitokana na ajali ya gari iliyotokea mnamo tarehe 2 Machi 2002. Jason alikuwa akitoka nyumbani kuliwahi basi la wachezaji wa Chievo Verona  kwani timu hiyo ya Chievo  ilikuwa ikijiandaa na mechi dhidi ya klabu ya Parma katika mchezo wa Serie A pale Estadio Ernio Tardin kunako mji wa Parma.Gari ya Jason iligongana na gari nyigine ndogo iliyokuwa na abiria wawili mmoja akiwa mwanamke ambaye alifariki papo hapo.Jason naye alifariki wakati akipelekwa hospitali ya Verona  kwa helikopta iliyokuja haraka kumchukua mara baada ya ajali hiyo lakini kutokana na majeraha makubwa aliyopata katika ajali hiyo Jason aliaga dunia kabla ya kufika hospitali.

Katika kuonesha kukuguswa na msiba huo,aliyekuwa waziri wa michezo wa wakati huo wa Congo DRC Timothee Moleka alisikika akisema kuwa “ni ngumu kulipokea jambo hili kwani dunia ilianza kumjua Jason na hakika alikuwa ni nyota mpya wa soka kwa Congo DRC”.Naye  mmoja kati ya waandishi wa habari za michezo nchini Congo Crispian Selemani hakuwa nyuma katika kulizungumzia tukio hilo kwa kusema kuwa “ni tukio la ghafla na la kusikitisha hakika ‘Simba’(jina la utani la timu ya taifa ya Congo DRC)ilikuwa ikimtegemea mno”.


Jason Nono Mayele alionesha uwezo mkubwa sana katika fainali za mataifa ya Afrika zilizofanyika nchini Mali kwani aliweza kushirikiana vyema na wachezaji kama Shabani Nonda aliyekuwa akichezea Monaco ya nchini Ufaransa na Tresor Lua Lua aliyekuwa Newcastle United ya nchini England.Na tukio kubwa katika fainali hizo ni timu yake ya taifa ya Congo DRC kuwatoa Tembo wa Afrika Magharibi timu ya Ivory Coast katika hatua ya raundi ya pili na kuingia robo fainali.
Katika kuonesha kuguswa na kifo chake,klabu ya Chievo Verona ya nchini Italia imesitisha kuitumia jezi Namba 30 iliyokuwa ikivaliwa na nyota huyo kwa heshima yake.

KUMBUKUMBU NA SPORTS GALLA

0 comments:

Post a Comment