
Klabu ya AC Milan ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha usajili wa mkopo wa kiungo mshambuliaji Ricardo Kaka.Mchezaji huyo aliye katika wakati mgumu katika klabu ya Real Madrid atajiunga kwa mkopo wa miaka miwili mpaka mwezi juni mwaka 2015.Katika mkataba wa sasa wa Kaka mpaka mwishoni mwa msimu huu,Kaka atakuwa akipokea kiasi cha euro milioni 3 ila kwa msimu ujao atapokea kiasi cha euro milioni 6 kwa mwaka.Tayari kocha Massimiliano Allegri ameshapewa baraka zote na viongozi wa Milan katika kukamilisha usajili huo.
0 comments:
Post a Comment