Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Wednesday, January 2, 2013

INTER MILAN WAMNYEMELEA LAMPARD

 
Klabu ya soka ya Inter Milan ya nchini Italia nayo imeingia katika vita ya kupata sahihi ya kiungo wa timu ya soka ya Chelsea Frank Lampard Jr.Kiungo huyo ambaye hatma yake haijulikani mpaka sasa kunako klabu hiyo ya Chelsea ya nchini England anatakiwa na vilabu vingi katika bara la Ulaya na Amerika(Marekani).Lampard mwenye miaka 34 anaweza kuondoka katika klabu hiyo ya darajani (Chelsea) endapo hatahakikishiwa mkataba mpya utakaomfanya aendelee kuwepo klabuni hapo.

Mkataba wa Lampard unaisha mwezi wa sita mwaka huu na hivyo kumfanya kuwa mchezaji huru pindi dirisha kubwa litakapofunguliwa mnamo mwezi wa saba mwaka huu.Lampard ambaye alijiunga na Chelsea mwaka 2001 anatakiwa pia na vilabu vya Lazio,LA Galaxy na PSG.Hii ni mara ya pili kwa klabu ya Inter Milan kumtaka kiungo Frank Lampard Jr kwani wamekwisha mtaka pia mwaka 2009 wakati Jose Mourinho akiwa kocha wa Inter milan.

0 comments:

Post a Comment