Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Wednesday, January 2, 2013

A.C MILAN ITARUDI TENA



Mnamo tarehe 16 Desemba 1899, Klabu ya A.C Milan ilianzishwa na raia wawili wa Uingereza Herbert Kilpin na Alfred Edwards ikihusisha mIchezo ya “football na cricket” Kutokana na mvutano uliosababishwa na sera ya usajili wa wachezaji wa kigeni mwaka 1908 iligawanyika na kuundwa klabu nyigine ya Inter Milan.
Katika kipindi cha nyuma ikiwa na wachezaji mahiri kama Franco Beresi, Paolo Maldini,Van Basten ,Inzaghi klabu ya AC Milan iliweza kushinda mataji mbalimbali kama UEFA Champions league, UEFA Super cup na mengineyo.Katika miaka ya karibuni A.C Milan imeshindwa kufanya vizuri katika michuano mbalimbali kitu ambacho kimechangiwa na vitu mbalimbali.
Kutowekeza katika soka la vijana,hili si tatizo kwa  Milan pekee bali vilabu vingi nchini italia.Vikosi vya vilabu hivi vimekuwa vikiundwa na wachezaji wenye umri mkubwa ,mfano katika kikosi kilichoanza na kutwaa ubingwa wa ulaya dhidi ya Liverpool mwaka 2007 ni wachezaji watatu tu ambao walikuwa chini ya miaka 30, Andrea Pirlo(27),Riccardo Kaka(25) na Gattuso(27) wachezaji wengine walikuwa wamevuka umri huo kama Maldini (39), Inzaghi (34) , Seedorf (31), Oddo (31) , Ambrosin (30) na Nesta (31)
Kuondoka kwa wakongwe ,mwanzoni mwa msimu huu 2012-2013 tumeshuhudia wakongwe kama Inzaghi, Nesta,Seedorf, Gattuso na Gianluca Zambrotta  wakiondoka.Hii imepelekea mabadiliko mengi katika safu mbalimbali hivyo itachukua muda kwa vijana waliopo kuunda kombinesheni bora kama ile ya Wa-Sweden Gunnar Gren, Gunnar Nordahl na  Nils Liedholm  miaka ya 1950 ama Ruud Gullit, Frank Rijkaard na Van Basten miaka ya 1980 kuondoka kwa wakongwe kumetoa nafasi kwa vijana kama Abate, El –Shaarawy, De-Sciglio , Acerbi na wengine.
Ukata wa fedha pia umepelekea Milan kuuza wachezaji wake nyota kam Zlatan Ibrahimovic na  Thiago Silva ambao wamejiunga na P.S.G.Hali hii imesababisha Milan kushindwa kununua wachezaji nyota kuziba nafasi  hizo, hivyo kuwa na safu mbovu ya mabeki wa kati huku katika ushambuliaji ikimtegemea zaidi Stephan El-Shaarawy.
Kushindwa kurudisha wachezaji nyota ambao Milan iliwatoa kwa mkopo kama vile Yoann Gourcuff aliyekuwa Girondins Bordeaux na baadae aliuzwa moja kwa moja .Wengi tuliamini kuwa angekuwa mbadala wa Ricardo Kaka aliyehamia Real Madrid.Pia makinda wengine kama Alexandre Merkel  aliyeko Genoa na Albert Paloschi (Chievo) nako kumeifanya klabu ya Milan iendelee na utamaduni wa kupoteza nyota wake wanaofanya vyema katika vilabu vingine(kwa mkopo) katika Serie A.
Katika kambi ya mazoezi Milanello vijana ndio wametawala hii inashiria kwamba klabu imedhamiria kuwekeza katika vijana hivyo tutarajie mafanikio siku zijazo.Klabu kama F.C Barcelona imepata mafanikio kutokana na kuwekeza katika soka la vijana hivyo kupata mafanikio kutokana na wachezaji  mazao ya academy zao.Kutoa nafasi kwa kina El-Shaarawy ,De sciglio, Acerb, Niang , Ganz na Bojan kutasaidia kuunda timu bora ya kiushindani. Hivyo naamini siku moja Milan itarudia makali yake.
Milan itarudi.
KEEP CALM & SUPPORT AC MILAN
Forza Milan
ANTONY MALIGANYA

0 comments:

Post a Comment