Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Thursday, January 10, 2013

IDFA YAANDAA KOZI YA WAAMUZI


 CHAMA cha Mpira wa Miguu Ilala (IDFA), kimeandaa kozi ya waamuzi itakayofanyika Januari 25, katika Shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa.

Kozi hiyo imeandaliwa kwa ajili ya kutafuta waamuzi wapya watakaoandaliwa vyema na kutumiwa siku za usoni, hasa kwa wale vijana wadogo, huku ikipangwa kufanyika siku za Ijumaa, Jumamosi na Jumapili kwa muda wa mwezi mmoja.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Chama hicho, Kanuti Daudi, alisema kwamba hadi sasa wameshajiandikisha vijana 20 wenye lengo la kushiriki kozi hiyo ya waamuzi.

Alisema bado nafasi zipo kwa wale wanaohitaji kozi hiyo, huku wakiamini kuwa italeta tija na kuinua michezo kwa kuwa na waamuzi bora.

"Tumeamua kuandaa kozi ya waamuzi kwa ajili ya kutafuta watu wa kuendeleza zaidi michezo hasa mpira wa miguu, kwa kuhakikisha mambo yanakwenda sawa.

"Naamini mambo yatakuwa mazuri hasa kwa wale vijana watakaojitokeza zaidi kwakuwa bado nafasi zipo na tunaamini watashiriki kwa wingi," alisema.

DRFA ni chama kinachopigania maendeleo ya mpira wa miguu Ilala, huku timu kongwe na zenye mashabiki wengi, ikiwamo Simba na Yanga zinazotokea katika eneo hilo.

0 comments:

Post a Comment