Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Sunday, December 30, 2012

CHELSEA YAIFUNGA EVERTON HUKU LIVERPOOL IKIIFUNGA QPR

 Are you listening, Roman? A Chelsea fan holding up a special banner at Goodison Park
Magoli ya mawili yaliyowekwa kimiani na kiungo nyota kunako klabu ya Chelsea Frank Lampard yaliipa ushindi timu hiyo ya Chelsea  na hivyo kuifanya isogee mpaka katika nafasi ya tatu ikiwa na point 38 huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi.Everton walianza mechi kwa kasi kwani kunako dk ya 1 kwanza tu ya mchezo kiungo Steven Pienaar alianza kufunga kwa upande wa Everton lakini baadaye kiungo wa Chelsea Frank Lampard alifunga goli  la kusawazisha katika dakika ya 42 na baadaye kunako dk ya 72 kiungo huyo alifunga tena na hivyo kuihakikishia ushindi klabu hiyo ya darajani.
Lift off: Luis Suarez fired Liverpool into the lead in the first half
Kule Loftus Road klabu ya Liverpool jana iliweza kuzinduka na kuibuka na ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya klabu ya QPR.Katika pambano hilo mshambuliaji Luis Suarez aliweza kufunga magoli mawili huku beki wa kati Daniel Agger akifunga goli lingine.

0 comments:

Post a Comment