Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Monday, November 19, 2012

NI MIAKA 20 YA KLABU BINGWA ULAYA


Ilikuwa ni Tarehe 25 November 1992  siku ya Jumatano mchezaji Daniel Amokachi alifunga goli katika dakika ya 17 katika pambano  kali na la kusisimua kati ya Club Brugge ya (Ubelgiji) dhidi ya CSKA Moscow ya nchini (Urusi) .Pambano hilo Ilikuwa ni kuashiria kuanza kwa mashindano mapya ya ulaya yaliyojulikana na yanayojulikana kama Klabu Bingwa Ulaya.Hakika bara la Ulaya lilikuwa katika nuru mpya katika soka kwani hapo kabla watu walishuhudia michuano hiyo ikijulikana kama Kombe la washindi barani Ulaya na tangu wakati huo wa 1992 mpaka sasa ni Klabu Bingwa Ulaya.Tarehe kama hiyo na mwezi kama huo mwaka huu (2012) itakuwa ni miaka 20 ya kuanzishwa kwa Klabu Bingwa Ulaya

Ni michuano ambayo ilikuwa na maswali mengi kwani baadhi ya vilabu vikubwa wakati huo vilikosekana kutokana na kutolewa katika hatua za awali kwenye miezi ya Septemba na Oktoba.Vilabu hivyo ni pamoja na Leeds United(England),FC Barcelona(Spain) bila kusahau VFB Stuttgartya nchini (Ujerumani) na hivyo watu kuamini kuwa michuano hiyo haiwezi kufana lakini kiukweli ilifana na inaendelea kufana sana.
Mwaka huu fainali ya UEFA au Klabu Bingwa Ulaya itafanyika katika dimba la Wembley ikiwa ni maadhimisho ya miaka takribani 20 tangu ijulikane kama Klabu Bingwa Ulaya.Mambo mengi au kuna mabadiliko mengi hapa katikati tumeyashuhudia lakini kubwa katika hayo ni matangazo ya televisheni kwa michauno hiyo kwani kwa kiasi kikubwa yamezidi kuleta msisimko na pia kuzidi kulipa utajiri shirikisho la soka Barani Ulaya pamoja na vilabu shiriki katika michuano hiyo.

Hivyo  kuelekea michezo ya kesho(Jumanne na Jumatano)ya Klabu Bingwa Ulaya,zimebaki siku saba tu za kusheherekea michuano hiyo tangu kuanzishwa kwake mwaka 1992.Ni miaka 20 ya michuano hiyo na hakika UEFA kama Shirikisho la soka Barani Ulaya wanastahili pongezi kwa hilo.

Gianni Ifantino
Katibu Mkuu UEFA

0 comments:

Post a Comment