Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Monday, November 19, 2012

HASHEEM ANAWEZA KUFANYA VYEMA NBA






Hakika alitabiriwa kuwa na maisha mazuri na marefu katika mpira wa kikapu nchini Marekani maarufu kama NBA kutokana na kushika nafasi ya pili katika ile iliyoitwa NBA College Draft ambayo hufanyika kila mwaka hasa kwa wale wanafunzi wa vyuo vikuu ambao hucheza mpira wa kikabu au Basketball.Si mwingine bali ni Mtanzania mwenzetu Hasheem Thabeet.

 Hasheem Thabeet alichaguliwa katika katika timu ya Memphis Grizzliers akiwa kama mshindi wa pil wa NBA draft ya mwaka 2009 na hapo ndipo maisha ya kijana huyu Mtanzania yalipoanza katika ulimwengu wa mpira wa kikapu.Tangu achaguliwe katika timu ya Memphis Grizzlies,Hasheem hakuwahi kufanya vizuri katika timu hiyo na hivyo kuzusha maswali mengi kuwa kama kweli ni huyu Haseem aliyeshika nafasi ya pili katika draft ya NBA au la.

Msimu huu wa kikapu wa mwaka 2012-13,Hasheem Thabeet amechukuliwa na timu ya Oklahoma City Thunder akitokea Houston Rocket timu ambayo hakufanya pia vizuri wakati akitokea timu ya Memphis Grizzlies.Wataalamu wa mambo wanasema kuwa kwa Hasheem Thabeet kwenda OklahomaCity Thunder kutamfanya kijana huyu wa kitanzania kung’ara katika Ligi Kuu ya kikapu nchini Marekani.

Kung’aa kwa Hasheem kutatokana na mambo mengi lakini kati ya hayo ni timu ya Oklahoma kuwa na uongozi mzuri uliojipanga katika kufanya mapinduzi makubwa katika timu hiyo na Ligi kuu ya NBA kwa ujumla chini ya kocha Sam Presti.Sam Presti ana kipaji cha kuendeleza vijana wenye vipaji kwa kuwachanganya na nyota wengine katika timu anayofundisha hivyo haitakuwa tabu kwa mchezaji mwenye futi 7’3 kama Hasheem kufanya vyema katika NBA.

Ni kweli mpaka sasa Hasheem hajawa na misimu mizuri katika NBA kwani hata rekodi zake zinaonesha hivyo.Kwa mfano tangu Hasheem aingie NBA ameanza michezo 16 tu huku muda mwingi akiutumia katika Ligi ya vijana inayotambulika kama D-League kuliko Ligi ya wakubwa yani Ligi ya Shirikisho(NBA).

Katika Ligi ya wakubwa yani NBA kwa mwaka 2009 mpaka 2012 Hasheem alikuwa na wastani pointi 2.2,rebounds 2.7,pasi za magoli 0.1,akiiba mipira kwa wastani wa 0.2 na akizuia mipira kwa wastani wa 0.9 kwa kila mchezo akiwa na ile PER(Players Efficenty Rating) ya 10.7.Hizi siyo takwimu mbaya kwa mchezaji wa kariba ya Hasheem na ndiyo sababu ya kocha Presti kuamua kumchukua Hasheem katika kikosi cha Oklahoma City Thunder.
Hasheem hatopewa majukumu makubwa sana katika timu ya Oklahoma bali kikubwa ambacho mwalimu Presti anakitegema  toka kwa Hasheem ni kucheza kama mlinzi katika kuzuia mpira inayokwenda katika goli au kikapu(shots) au rebounds kwa maana ya ile mipira inayozagaa katika lango la Oklahoma. Sidhani kama pia atakuwa akianza katika kikosi cha kwanza kikiwa na nyota kama Kelvin Martin,Kelvin Durant na Russel Westbrook.

Akiwa na timu ya Connecticut hakufanya mabo mengi sana zidi ya hayo niliyoyataja.Hakuitaji kuwa mfungaji alikuwa bora katika eneo alilocheza la ulinzi.Ni vizuri kukumbuka kuwa kikubwa kinachomfanya mchezaji kuwa bora katika NBA ni kujituma na kucheza kwa bidii na hilo halina shaka kuwa Hasheem anaweza kulifanya akiwa na Oklahoma City Thunder
Bottom of Form


0 comments:

Post a Comment