Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Thursday, October 25, 2012

FRANK RDJIKAAD ATAJWA KUMRITHI ALLEGRI AC MILAN

Frank Rijkaard Saudi Arabia
Wakati hali ikiendele kutokuwa shwari kunako klabu ya AC Milan,mchezaji wa zamani wa klabu hiyo na kocha wa zamani wa klabu ya FC Barcelona Frank Ridjikaad anatajwa kama mrithi wa kiti cha moto cha kocha wa sasa wa klabu ya Ac Milan Massimiliano Allegri.Taarifa zisizo rasmi zinasema kuwa mmiliki wa klabu hiyo ya AC Milan alikwisha mteua kocha Ridjikaad kabla ya mechi ya Malaga na Ac Milan hapo jana kunako Ligi ya Mabingwa Ulaya lakini makamu wa Rais wa klabu hiyo Adriano Galliani amekuwa akimtetea Allegri.

Ridjikaad anayeifundisha timu ya Saudi Arabia hivi sasa ni miongoni mwa makocha wanaotajwa kuchukua nafasi ya kocha wa sasa Massimiliano Allegri sambasamba na makocha wengine kama Pep Guardiola,beki wa zamani kunako klabu hiyo Alexandre 'Bill' Costacurta na kocha msaidizi kunako kikosi hicho kwa sasa  Massimo Tonato.

0 comments:

Post a Comment