Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Saturday, September 29, 2012

SUAREZ AMLIPA VAN PERSIE

Hot shot: Luis Suarez scores his first goal
Mshambuliaji Luis Suarez jana alikuwa shujaa wa Liverpool mara baada ya kuifungia timu yake magoli matatu'hat trick' katika pambano lililofanyika pale Carrow Road dhidi ya Norwich City.Suarez aliyekuwa mwiba hapo jana akiongoza mashambulizi pamoja na makinda Suso na kinda mwingine Raheem Sterling walikuwa katika kiwango chao bora kabisa dhidi ya Norwich.
On target: Grant Holt of Norwich City
Ulikuwa ni ushindi wa kwanza kwa Liverpool mara baada ya mechi tano na wa pili mfululizo katika juma hili ambapo majogoo hao wa Anfield wakiwafunga Norwich kwa magoli 5-2.Magoli hayo yakitiwa kimiani na Luis Suarez katika dakika 2,38,57 huku kiungo Nuri Sahin naye nyota yake ikizidi kung'aa baada ya kuifungia Liverpool goli lake la pili la msimu katika dakika ya 47 kabla ya nahodha Steven Gerrad kuhitimisha karamu ya magoli katika dakika ya 68.
Magoli kwa upande wa Norwich yalifungwa na Morrison dakika 61 na Grant Holt dakika ya 87 aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Jackson.

0 comments:

Post a Comment