Wayne Rooney akielezea goli lake katika kitabu chake
alichokizindua hivi karibuni kinachoitwa My decade in the premier league ambacho
mwendelezo wake unachapishwa pia na gazeti
la the mirror.Rooney maarufu kama “Wazza” alifunga goli hilo dhidi ya
wapinzani wao wakubwa katika jiji la Manchester na hao sio wengine ni
Manchester City.Hakika lilikuwa ni goli bora kabisa sio kwa Rooney pekee bali pia
kwa Manchester United lakini pia hata
kwa ligi kuu yenyewe pale nchini Uingereza. Ilikuwa ni mwezi wa pili dakika ya
77 mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uingereza na timu ya Manchester United alipofunga
goli hilo maarufu kama tik-tak na kuipa timu yake ushindi wa 2-1.
Rooney anasema goli lile ilikuwa ni tamu na ni maalumu kwa
majirani zetu wanopiga makelele.Utamu wa goli lenyewe sio tu kwamba unachagizwa
na mechi ya baina ya watani wa jadi bali ni ukweli kwamba lilikuja wakati ambao
Rooney ametoka kushusha presha za mashabiki miezi miwili iliyopita baada ya kusaini mkataba mpya baada takribani juma zima kuhusishwa na kuihama United.Anaendelea anasema hisia za kuifungia
Manchester united goli kama lile mara zote huwa ni kubwa sana lakini ni kubwa
zaidi kwasababu nimewafunga Manchester City.Ansema jinsi nilivyojisijisikia
kama ningepata nafasi ningejitengenezea kinywaji chenye nguvu sana mfano wa
konyagi hivi au banana kwa hapa kwetu sijui kwao ingekuwa nini.
Ansema mara nikahisi mapigo yangu ya moyo yananienda mbio
mara nikahisi yamerudi katika hali yake naona kila kitu kipo sawa ila nasikia
sauti kubwa inayoumiza masikio yangu jasho linashuka kwenye shingo yangu na
huku jezi yangu ukiwa imejaa matope,mara naskia makelele juu yangu mara watu
wanavuta jezi yangu na mapigo ya moyo nayo yakienda yakiongezeka kifuani
kwangu.Nasikia mashabiki wakiimba jina labu Rooney Rooney Roooney Roooonee-
Rooney na hakika hakuna hisia bora duniani kama hizi.
Anendelea anasema niliposimama huku kichwa kimetazama juu na
mikono yangu nimeitawanya nasikia makelele na maneno ya chuki kutoka kwa
mashabiki wa Manchester City yalikuwa ni kama umeme ambao hauzunguki yalikuwa
na maneno makali yaliyochanganyika na matusi kebehi na vitisho mbali mbali
lakini sikujali sana kwasababu najua kiasi gani wananichukia na hata mimi
najisikia vivyo hivyo pindi ninapofungwa. Lakini mimi ni Wayne Rooney nimecheza
ligi kuu kwa miaka kumi sasa tangu 2002 kwa hiyo nina uzoefu lakini kikubwa nimefunga
goli bora na muihimu pengine kuliko yote
msimu mzima kwa upande mwekundu wa mji na kuwatahadharisha na wapinzani wengine
kwamba tunaenda kuchukua kombe lingine.

0 comments:
Post a Comment