Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Wednesday, September 5, 2012

ASAMOAH NA JUVENTUS


ASAMOAH ANA NAFASI KATIKA KIKOSI CHA JUVENTUS?
“Mchezaji bora tunayemtafuta ama kumsajiri siyo yule mwenye jina kubwa au anayeuzwa kwa fedha nyingi sana.Tunachomaanisha kwa mchezaji bora ni Yule ambaye atatuongezea ufanisi na au kufanikisha ushindi katika kikosi cha Juventus”.Maneno haya anayazungumza mtendaji mkuu(CEO) wa klabu ya Juventus anayejulikana kama Giuseppe Marrota au waweza kumwita Peppe Marrota.
Klabu ya Juventus imefanya usajiri wa wachezaji kadhaa msimu huu wa Serie A kama Mauricio Isla,Nicola Leali,Richmond Boakye na bila kmsahau kiungo mchezeshaji Kwado Asamoah.Wachambuzi wengi wa mambo na wapenzi wa Juventus wanajiuliza kuwa Je,Kwado Asamoah ataweza kupata namba katika kikosi cha kwanza cha Juventus?na Je,nafasi yake katika kikosi cha Juventus ipoje?
Kwa walioitazama mechi ya Supercoppa Italiana kati ya Juve na Napoli watakubaliana na mimi kuwa Kwado Asamoah ameleta changamoto mpya katika kiungo cha Juventus ambacho kwa muda mrefu sasa kimekuwa na viungo bora kabisa watatu Ulaya ambao ni Arturo Vidal,Andrea Pirlo na Claudio Marchisio.Ujio wa Kwado pia utalifanya Juve iwe na uchaguzi wa mifumo mbalimbali tofauti na wa sasa unotumika mpaka na kocha anayeshikilia nafasi ya Antonio Conte ambaye amefungiwa na chama cha mpira wa miguu nchini Italia(FIGC) namzungumzia Massimo Carrera.
Nilikuwa nikijiuliza pia kuwa itakuwaje kama kiungo maestro Andrea Pirlo ambaye anaonekana kama uti wa mgongo wa klabu hiyo ya Turin anakosekana katika kiungo cha Juventus?Je,Juve  watakuwa na nguvu ama uwezo kama walionao wakiwa na kiungo huyo?Nasema hivyo kwa sababu Pirlo alicheza mechi 37 katika msimu uliopita wa Serie A katika umri wake wa miaka 34.Na alionekana kuwa na msaada mkubwa sana katika kiungo cha Juve pamoja na kuwepo kwa viungo wengine kama Simone Padoine,Emanuel Giacherrine,Arturo Vidal na Claudio Marchisio.
Kwa kipindi kirefu sana klabu ya Juventus haijapata mchezaji wa kariba ya Asamoah hasa katika idara ya kiungo ambaye atakuwa na uwezo wa kucheza nafasi zaidi ya moja uwanjani na wakati huo huo akiwa na uwezo wa kupiga pasi katika ile robo tatu ya lango la timu pinzani.Si Arturo Vidal,Marchisio wala Pirlo wenye uwezo wa kucheza nafasi zaidi ya moja kama aliokuwa nao Asamoah na hivyo Asamoah kujidhiirisha kuwa ni mmoja kati ya wachezaji bora ambao Juve wamewasajiri msimu huu.

Uwezo wa Asamoah unafananishwa na uwezo wa wachezaji waliopita katika klabu hiyo kama Edgar Davis na Didier Deschamps ambao walikuwa na uwezo wa kucheza nafasi zaidi ya moja uwanjani.Kwa mfano Edgar alikuwa na uwezo wa kucheza kama beki wa kushoto vizuri,kama kiungo mkabaji,kama kiungo wa kati na kama winga pale ilipolazimu.
Add caption
Asamoah ni aina ya viungo wanaoweza kusogea toka eneo alilopangiwa katika majukumu uwanjani mpaka katika maeneo ya hatari ya timu pinzani na hivyo kumfanya awe katika nafasi nzuri sana katika kupata nafasi kikosi cha kwanza cha klabu hiyo maarfu kama La Vecchia Signora(Kibibi kizee cha Turin).Asamoah anakumbukuwa mno na mashabiki wa klabu ya Udinese maarufu kama Pundamilia wadogo(Zebrette) kwa namna alivyoweza kutengeneza kombinesheni bora kabisa katika klabu hiyo na Serie A kwa ujumla kwa namna alivyoweza kushirikiana na viungo bora kabisa waliowahi kuichezea klabu ya Udinese si wengine bali ni Gaetano D’Agostino na Gokhan Inler.
Ni mchezaji mdogo kiumri na hakika mategemeo ni mengi sana kwa mashabiki wa Juventus kwa huyu kijana Kwado Asamoah.Ingawa angalizo kwa mashabiki na wadau wa klabu hiyo ni kuwa Asamoah anahitaji muda ili kuweza kuzoea mazingira vyema ya uwanja(Juventus Areana) au viunga vya mazoezi vya klabu hiyo vinavyojulikana kama Juventus centre.Akipewa nafasi na kuaminiwa,Asamoah ataendelea kuifanyia Juve mambo makubwa kama yale tulioyaona katika mechi dhidi ya Napoli katika lile pambano la Supercoppa Italiana pale Beijing China.
Kila la kheri  Kwado Asamoah katika maisha uliyoanza kunako klabu ya Juventus.

0 comments:

Post a Comment