Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Thursday, September 6, 2012

UWANJA WA ZIMBRU WAMPA WASIWASI ROY HOGSON




 
 Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uingereza maarufu kama the three Lions Roy Hugson ameonyesha wasiwasi wake na uwanja wa Zimbru uwanja wa nyumbani wa Moldova. Uwanja wa Zimbru ndio uwanja wa nyumabini wa Moldova utakapofanyika mchezo wa kufuzu kombe la dunia baina yake na Uingereza siku ya ijumaa.Hogson na kikosi chake wameamua kusafiri mapema kwenda Moldova ili wakapate nafasi ya angalau kufanya mazoezi ili wasije wakashangazwa siku ya mchezo.Uwanja wa Zimbru inasemekana ni mdogo na majukwaa yake yapo karibu na uwanja wa kuchezea na wanasema kiwango hiki sio cha ligi kuu labda ligi daraja la pili maarufu kama( Champioship). Hata beki wa kutumainiwa wa  Uingereza pamoja na Chelsea Gary Cahill “anasema sehemu yenyewe inaahidi na kuonyesha kabisa sio nzuri na ndio maana tumesafiri mapema kuzoea uwanja”

Hogson anasema kuna mambo kibao ya kutegemea unapoenda sehemu na nchi kama Moldova anasema unaweza ukajiuliza maswali  kama je uwanja utakuwaje?au je hali ya hewa kwa ujulma itakuwaje? au je vipi sehemu wenyewe ya kuchezea na vipi kuhusu ina ya wachezaji unaoenda kukutana nao? kwa hiyo lazima pia tuangalie wachezaji waliopo na jinsi gani tinajiandaa na  kwa ujumla kuna mambo mengi ya kuangalia kuelekea mchezo wenyewe.Anasema najua katika kikosi changu kuna mawazo kibao kuhusiana na timiu tunayoenda kukutana nayo na wengine watasema sio timu ya kutisha lakini hatuwezi kwenda kwenye mchezo huo na mawazo kama hayo lazima tuwe makini sana.

Lazima twende huku tukijua fika kwamba Moldova sio timu ya kubeza kwani michezo yao ya mwisho ya kufuzu walitoa sare na kufungwa tena kwa ushindi mwembamba dhidi ya Uholanzi.















0 comments:

Post a Comment