Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Saturday, September 15, 2012

PREVIEW:ARSENAL VS SOUTHAMPTON



 

Ni mpambano kati ya washika bunduki au washika mitutu wa London Arsenal na watakatifu au the Saints  hawa sio wengine ni Southampton mchezo ukipigwa katika dimba la Emirates siku ya Jumamosi majira ya saa 9:45 alasiri.Ni mchezo unaosubiriwa kwa hamu sana na mashabiki wote mwenyewe nikiwemo kwani ni mchezo unaohidi kila viashiria vya soka safi na ya kuvutia kutokana na timu zote kupenda soka ya kushambulia na ufundi mwingi. Kuna vitu vingi sana binafsi vinanivutia kuhusu the Saints au watakatifu achilia mbali kwamba bado hawa japata pointi hata moja lakini soka safi ya kujiamini hasa walipocheza na mabingwa watetezi Manchester City na Manchster United ni ishara tosha ya aina mchezo unaoutarajia pale Emirates.Katika michezo yote miwili walifika katika hali ya kuonekana wanashinda mchezo lakini uzoefu ukwaadhibu wakipoteza kwa matokeo yanayofanana ya 3-2 lakini bado nina imani watakatifu wamekuja na wataishi milele.

ARSENAL.
 Reasons to be cheerful: Arsenal have made a solid if unspectacular start to the season
Arsenal kulekea katika mchezo huu wanachagizwa na ushindi wa 2-0 pale Anfield kabla ya wiki ya mechi za kimataifa shukrani ziwaendee Lukas Poldoski na Santi Carzola kwani wote walifanikiwa kufungua akaunti zao Bacrays pale kunako ligi kuu nchini Uingereza.
Lakini kikubwa cha kuvutia zaidi ni swali kwamba je Arsenal wataendelea kulinda vyavu zao zisiguswe? Arsenal mpaka sasa wameshacheza michezo mitatu ya kwanza ya ligi  bila kuruhusu goli hata moja  nakuifikia rekodi ya klabu baada ya miaka 88 na kama watamaliza mchezo huu bila kufungwa watafikisha mchezo wa 4 bila kuruhusu wavu wao kuguswa na kutengeneza rekodi mpya ya Arsenal.

Arsenal pia kuelekea mchezo huu ina wasiwasi wa kukosekana kwa baadhi ya nyota wake kama Abou Diaby  na Theo Walcott ambao wamepata maumivu na timu zao za taifa laikini pia itategemea na vipimo vya mwisho vitakavyosema.Majeruhi wa muda mrefu wataendelea kukosekana kama Jack Wilshere,Thomas Rosicky na Bacary Sagna na mchezaji pekee ambaye atarejea ni Wojciech Zscesny baada ya kupona maumivu ya mgongo hivyo ikimaanisha atachukua nafasi ya Vito Mannone golini.

SOUTHAMPTON.
 
Kurudi kwa watakatifu katika daraja la ligi kuu la premier nchini Uingereza kumeshuhudia wakitupwa katika shimo refu kabisa lenye timu kama Manchester City, Manchester United na Arsenal kwa pamoja katika mechi zao za ufunguzi wakiambulia pointi 0 mpaka sasa.Lakini Kocha wa Southampton Nigel Adkins anasema wanayachukulia matokeo haya kwa mtazamo chanya na wanaimani kwa uwezo walioonyesha katika michezo yote watabaki ligi kuu.Southampton wanaenda London kusaka pointi yao ya kwanza ligi kuu japo wanakumbana na ukweli kwamba timu nyingi amabazo zimepanda daraja na kupoteza mechi zao  tatu za kwanza zimishuka daraja.
Moving on: Alex Oxlade-Chamberlain and Theo Walcott (right) were both trained at Southampton 
Alex-Oxlade Chamberlain na Theo Walcott ni mazao yanayotokana na Shule ya soka ya Southampton lakini kutokana na Walcott kuumia Chamberlain ndio mwenye nafasi kubwa ya kukutanana timu yake ya zamani.Nigel Adkins kocha mkuu wa Southampton  anamuongelea the Ox anasema najivunia sana kuona maendeleo ya Alex tangu ametuacha na kila mtu lazima ajivunie kwa sababu ametokana na mfumo wetu.Mara zote ukimtazama unafurahi hatukufurahi alipoondoka na unataka afanye hivyo kwa timu ya taifa ya Uingereza ila tunataka awe na siku mabaya tutakapokutana. Mchezaji ambaye amevunja rekodi ya uhamisho kwao  Gaston Ranirez amekamilisha taratibu zote anaweza akapata nafasi katika mchezo huu.
UKWELI KUHUSU MECHI.
ARSENAL.
Arsenal hawajapoteza michezo 17 nyumbani wakicheza na Southampton tangu wafungwe 1-0 mwezi Novemba 1987 na katika msimu wa mwisho ambao Southamton walikuwa ligi kuu 2004/2005 mechi zote ziliisha kwa sare.

Arsenal hawajashinda michezo 4 ya ligi nyumbani ni mingi zadi tangu wahamie Emirates kwa kipindi cha miaka 17 na mara ya mwisho walienda michezo 5 ya ligi bila ushindi  nyumbani ilikuwa msimu wa 1994/1995.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya Arsenal wameanza ligi michezo mitatu bila kufungwa hata goli moja.Portsmouth ndio timu pekee ya ligi kuu kwenda michezo 4 bila kufungwa hata goli moja msimu wa 2006/2007.

Wakati Theo Walcott anabaki kuwa mchezji mdogo kabisa kuwahi kuiwakilisha Arsenal ligi kuu akiwa na umri wa miaka 16 na siku 143,Alex Oxlade Chamberlain ameshaifungia Soputhampton magoli 9 katika michezo 36.

Santi Carzola ndio kiungo anayengoza kwa kupiga pasi sahihi ligi kuu nchini Uingereza katika eneo la hatari la mpinzani zikiwa na usahihi wa 88%.

KIKOSI CHAWEZA KUWA HIVI.
Sczcesny
Jenkinson, Vermaelen, Koscielny, Gibbs
Diaby, Arteta, Cazorla
Oxlade-Chamberlain, Giroud, Podolski

SOUTHAMPTON.
Watakatifu ndio timu pekee ligi kuu mpaka sasa hawajapata pointi hata moja wakiwa wameshapoteza michezo miwili kwa 3-2 katika michezo mitatu ya mwanzo.

Huu ni msimu wa 13 katika 15 wameshindwa kupata ushindi katika michezo yao mitatu ya mwanzo ya ligi na wameshapoteza michezo yao 4 ya mwanzo ya ligi msimu wa 1998/1999 ambapo walimaliza ligi nafasi ya 17.

Waatakatifu walikuwa mabingwa wa ligi daraja la kwanza nchini Uingereza maarufu kama Championship wakifunga magoli 85 lakini 4 tu ndio yaliyofungwa nnje ya eneo la mita 18.

Japo wanashika nafasi ya mwisho katika msimamo wa ligi lakini watakatifu wamefunga magoli mara 2 ya yale Arsenal  2.

KIKOSI CHAWEZA KUWA HIVI.
K Davis
Clyne, Hooiveld, Fonte, Fox
Schneiderlin, S. Davis, Ward-Prowse Puncheon, Lambert, Lallana









0 comments:

Post a Comment