Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Monday, September 24, 2012

HATIMAYE EVRA AKUBALI YAISHE



 Key moment: Patrice Evra shakes hands with Luis Suarez
 Ni siku iliyokuwa imejaa matukio mengi ambayo kila mtu na kila shabiki yalimsisimua na hakika ilikuwa ni mechi ilyokutanisha wanaume kweli kweli.Achilia mbali mpambano wa wachezaji uwanjani ni vita kweli kweli lakini pia sikiliza nyimbo na mapambio ya mashabiki wa timu zote mbili hii inatokea mara chache sana katika msimu.Matukio yaliyojawa na hisia kali pamoja na uhasama yalikuwa ni mengi lakini yote kwa yote hatimaye Patrice Evra amekubali kushikana mkono na Luis Suarez.Tukio hili lilishidikana kwa takribani miezi 7 iliyopita lakini tukio la Hillsborough limemgusa kila mtu na Evra” anasema ilikuwa ni vizuri kusahau nyuma tofauti zetu na kupisha umuhimu wa siku yenyewe”.

 Bury the hatchet: Evra and Suarez acted as requested
Anaendelea anasema ilikuwa ni mechi kubwa baina timu timu kubwa na kitu muhimu ilikuwa kuonyesha heshima kwa mashabiki waliopo na wale waliotutoka.Kulikuwa na janga kubwa katika historia ya klabu lakini watu walikuwa wanaongelea suala la kushikana mikono ambalo mimi sioni kama ni muhimu zaidi ya historia ya klabu.Evra anasema yote kwa yote nimefurahi sana kwasababu amenishika mkono na kuonyesha kwamba wote tunaziheshimu familia zilizopoteza jamaa zao na ilikuwa ni siku ngumu sana.

0 comments:

Post a Comment