Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Monday, September 24, 2012

CLASSY CARZOLA.Arsenal wameizulumu Malaga


 Little master: Santi Cazorla has made big impression
 Manchester United wanaweza wakawa wamemnunua Robin Van Persie kwa £24,Chelsea wamemnunua Eden Hazard kwa £32 ,Oscar kwa £ 25  lakini Santiago  Rodriguez Carzola hakika Arsenal wameizulumu Malaga.Ameigharimu arsenal kiasi cha £15 na hayo sio maneno yangu ni maneno ya kiungo wa Swansea Miguel Perez Cuesta a.k.a Michu kiungo ambaye amecheza na Carzola kweye Shule ya soka ya Oviendo. Achilia mbali Mbali uwezo wake wa kuusoma mchezo,kukimbia na mpira umbali Fulani,kupiga mashuti yanayolenga lango,kuwa na muono na pasi sahihi pamoja na stamina ya kutosha lakini kubwa ni kuweza kufanya haya yote kwa kutumia miguu yake yote kwa 100%.

Achilia mbali ubahiri wa mzee Wenger lakini kwangu Carzola anabaki kuwa mchezaji bora katika ligi kuu ya premier aliyesajiliwa msimu huu.Soka la Ulaya siku hizi limeharibiwa na pesa lakini kama umetazama mchezo wa jana baina ya Arsenal na Manchester City unaweza ukapanga mwenyewe Carzola  anunuliwe na alipwe kiasi gani lakini sio £15 pesa iliyomleta Alex-Oxlade Chamberlain Arsenal.Ubora wake huwezi kuutofautisha na wa Yaya Toure na David Silva  wanaolipwa £200,0000 kwa juma na kuna baadhi ya vitu ambavyo vinamtengeneza Carzola hawana.

 On the ball: Cazorla will face a big test at Manchester City
 Huyu jamaa ni hatari sana na bahati nzuri amekutana na mtu mwingine hatari vile vile Profesa anayeweza kujua wapi mchezaji sio tu atacheza bali atacheza na kuweza kupata ujazo wa kipaji chake na huyu si mwingine ni mzee Wenger. Carzola mwenyewe anasema nilijua nakuja kucheza pembeni kama nilivyozoea  lakini nimewekwa sehemu ambayo nahisi nilipaswa kucheza wakati wote huko nyuma.Carzola muda wote wa kucheza soka amecheza sana pembeni lakini kwa sasa anaecheza akiwa mchezaji huru uwanjani eneo ambalo zamani alikuwa akicheza Fabregas.
 Class act: Santi Corzola (bottom row, far left) with his Oviedo youth team-mates, including new Swansea striker Michu (centre bottom)
 Santiago Carzola sio tu kwamba amewafanya Arsenal wamsahau Cesc Fabregas aliyetimkia Barcelona lakini pia ameongeza ubora kwenye kiungo ya Arsenal na kuwafanya wawe katika nafasi nzuri ya kumaliza ukame wa vikome Emirates. Kurejea kwa Jack Wilshere,Abou Diaby,Thomas Rosicky, Emanuel Frimpong na uwepo wa Mikel Arteta,Aaron Ramsey,Frasis Cocuelin na Alex Oxlade Chamberlani kumemfanya Wenger kufika hatua ya kusema kwa ubora na idadi ya viungo nilionao ni mchanganyiko ambao sijawahi kuuona wala kuwa nao  muda wate niloishi hapa.

0 comments:

Post a Comment