Maneno haya yanamtoka Muingereza David Haye baada ya
kushuhudia Vital Klitschko akimchakaza kwa kumchanana vibaya juu ya jicho Mjerumani Mannuel Charr raundi ya
pili katika uwanja wa olympic Arena
jijini Moscow. David Haye anasema Vitali
mwenye umri wa miaka 41 kaka wa Wladimir Klitschko japo ameshinda lakini
nimeona mapungufu mengi kwenye kuzuia ama kujilindana na kama akikutuna na mimi
nina uhakika hawezi kuvuka hata raundi ya sita.Nimesikitishwa sana na kiwango
cha Vitali na ningependa kupambana naye na kummaliza.Anaendelea anasema Vitali
ni mpiganaji lakini nina uhakika nitakopomrushia makonde hawezi kuyazuia na
hakika leo hakucheza vizuri na amejiaibisha mwenyewe.
David Haye baaada ya kusamehewa adhabu yake ya kufungiwa baada ya kuleta vurugu mwezi wa pili pale
Darek Chisora aliposhindwa kwa pointi na Vitali analitafuta pambano na Vitali
kwa nguvu zote hasa baada ya mwaka jana kupigwa na Mdogo wake Wladimir
Klitschko na hivyo anafuta nafasi ya kulipiza kisasi.Haye anasema pambano lake
na Vitali ana uhakika sio tu kwamba litakuwa kali na lakusisimua lakini pia
litakuwa pambano bora katika historia ya masumbwi duniani hasa kutokana na
ukweli kwamba amerudi katika ubora wake baada ya kumshinda Chisora mwezi wa
saba. Pambano kati ya David Haye na
Vitali Klitschko ni pambano ambalo linasubiriwa kwa hamu katika ulimwengu wa
masumbwi duiniani na linatarajiwa
kufanyika mwezi wa pili mwakani lakini likitegemea zaidi kama Vitali atashindwa
katika kinyanga’nyiro cha kuingia Bungeni nchini Ukraine.
0 comments:
Post a Comment