Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Monday, September 10, 2012

ABOU DIABY KUWAKOSA BELARUS KESHO


 
 Unaweza ukasema chochote lakini Habari hizi ni bundi ambaye ameanza kulia kwenye nyumba ambayo ndio kwanza imenza kusahau habari za misiba.Habari hizi sio mbaya kwa Abou Diaby peke yake bali pia Arsene na Arsenal kwa ujumla  kwani ndo kwanza amerudi kutoka majeruhi akiwapa ushindi Arsenal na Ufaransa kwa pamoja.Abou amepata tatizo la msuli mdogo na hii inamaanisha anaweza akakosa mchezo wa nyumbani wa Ufaransa dhidi ya Belarus  na pia mechi ya ligi kuu ya premier dhidi ya Southampton kwenye dimba la Emirates.

Habari hizi zinakuja wakati ambao Didier Deschamps amesifia uwezo wa Diaby akiwa amefunga goli pekee katika ushindi wa Ufaransa dhidi ya Finland katika kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia nchini Brazil akisema ni kiungo ambaye amekamilika.Akieleza majeraha hayo kocha wa Ufaransa Deschamps anasema amepata maumivu mabaya ambayo yanamfanya asitembee kwa uhuru na leo hatutamruhusu kufanya mazoezi.Anaendelea anasema sio yeye tu hata Gael Clichy watapata wakati mgumu kuweza kuwahi mechi dhidi ya Belarus.

0 comments:

Post a Comment