Abou Diaby amepitia kipindi kigumu sana katika maisha yake
ya soka akiandamwa sana na majeruhi.Nakumbuka pambano fulani pale Emirates
Arsenal wanacheza dhidi ya Newcastle United alitolewa nje kwa kadi nyekundu
baada ya Joe Barton kumchezea vibaya lakini yeye aligeuka David Haye.Lakini
unaweza kuwa kwenye akili ya Diaby kwamba sio tu alikuwa anawaza kurudi tena
kwenye kitanda cha matibabu lakini pia nina imani alimwita Joe Barton
mshirikina kama sio mchawi maana alionekana kabisa alijua alichokuwa
anakifanya.
Lakini Diaby sasa amerejea na amenza kuonyesha kile watu
walichokuwa wanakitegemea toka kwake kwa Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa. Na
anasema huu ni msimu muhimu sana kwangu
nafanya kazi kubwa sana kuweza kupata mafanikio kuliko wakati mwingine wowote
na nataka kumuonyesha kila mtu kwamba ninaweza.Nimefikia umri na wakati katika
maisha yangu ya soka kuuonyesha uwezo wangu kwa muda mrefu na kusahau kila kitu
nyuma na hakika iliandikwa nitarejea na wakati wa kuifanyia makubwa Arsenal ni
sasa kama sio sitaweza tena.
Uwezo alionyesha kwenye mechi dhidi ya Liverpool sio tu
kwamba uliipa Arsenal ushindi wa kwanza kwa msimu huu lakini pia alipata tuzo ya
mchezaji bora wa mchezo na hatimaye kurudishwa katika timu ya taifa ya
Ufaransa.Katika mchezo huo Diaby alifunga goli pekee dhidi ya Finland kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia zitakozfanyika nchini Brazil
2014.Kocha wa Ufaransa wa sasa Didier Deschamps naye hakubaki nyuma kumsifia
Diaby anasema sio tu kwamba ni kiungo mwenye kila ubora lakini pia nafahamu kwamba ni kiungo aliyekamirika. Naye kiungo
mwenzake Rio Mavuba anasema pengo lake
kwenye kikosi ni vigumu kuliziba emethibitisha tena ubora wake na ameweza
kizibiti presha ya mchezo na nina imani ataendelea hivyo.
0 comments:
Post a Comment