Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Tuesday, August 21, 2012

WATAKATIFU WAMERUDI NA WATAISHI MILELE











Southampton au 'the Saints' au watakatifu kwa kikwetu hakika wanaonekana hawakuja na kuondoka bali wataishi milele.Wakirudi daraja la premier la ligi kuu nchini Uingereza baada ya miaka saba hakika ulikuwa ni ukaribisho mzuri kwao kukutana na watetezi wa taji matajiri wa jiji la Manchester au wanapenda kujiita 'the Citizen' au kikwetu wananchi ama raia.Kikubwa kilchonifurahisha kwenye mechi hii ni jinsi watakatifu walivyokuwa sio waoga, walivyokuwa wanafunguka  na jinsi walivyokuwa wanashuka na kujenga   mashambulizi yao ya kushtukiza(counter attacks) ambayo yalikuwa ya kujiamini sana.Kumbuka walikuwa Etihadi uwanja ambao City wana rekodi ya kutopoteza michezo 30 wakishinda 28 na msimu uliopita wakifungwa magoli 12 tu chini ya nahodha Vicent Company lakini watakatifu wakafunga mabao mawili.



Natamani sana kuwaona watakatifu wakicheza kwenye ligi yao kwa maana ya kuchea na vilabu vya daraja lao vilabu ya kariba ya  Swansea,QPR,Norwich,Wigan,Aston Villa,Stoke City,Reading na West Ham.Kocha Adkins alionyesha kwamba ana watu ambao wanaweza kuipa shida beki ya timu yoyote atakayokutana nayo.Akianza  kwa kumuacha benchi Rickie Lambert na kuanza na Jay Lodriguez kutoka Bunrey ambaye ni usajili pekee walioufanya mara tu baada  ya kupanda daraja bado watakatifu walionekana hatari pale Etihad.Rickie Lambert mfungaji bora wa ligi daraja la pili (championship) msimu uliopita na pia tayari akiwa ameshawafungia watakatifu mabao 88 katika michezo 158 ilimchukua dakika 4 tu kufungua akaunti yake ya magoli katika ligi kuu nchini Uingereza na pengine kuwemo katika orodha ya wafungaji bora msimu huu akiwa na miaka yake 30.

Japo City ushindi wao katika mechi  tatu zilizopita wameupata huku wakikaribia kupoteza mchezo lakini goli la Rickie Lambert lilifanya matokeo kuwa 2 -1 na kuwafanya watakatifu wahisi sio tu kupata point za kwanza bali pia kuvunja rekodi ya Etihadi kabla ya Nasri na Dzeko kufanya matokeo kuwa 3-2  wakitanguliwa na Tevez .Uelewano wa Carlos Tevez na Kun Agguero hasa katika mechi sita za mwisho msimu uliopita zingetosha kuitisha ngome ya timu yoyote.Hata hivyo  Robert Mancini hakuhitaji mguu wa Agguero uliompatia kombe msimu uliopita ili kufungua mvinyo kwani aliumia mapema  safari hii  alihitaji zaidi filimbi ya mwisho ya Howard Webb  manake watakatifu walikuwa wanakuja kila dakika.

Kwa Southampton  kikubwa kilichokuwa kinawazuia kurudi kwao misimu saba iliyopita ni kuuzwa kwa baadhi ya nyota wake ambao walionekana ni wakubwa kuliko watakatifu.  Unakumbuka nyota kama kina Bale,Theo Walcott pamoja Alex-Oxlade Chamberlain lakini  Adkins ndani ya misimu mitatu amefanya kazi kubwa kuwatoa daraja la tatu mpaka ligi kuu kitu ambacho sio tu kimeirudisha premier league pale St.Marry's bali pia ameweza kulinda kazi yake kama kocha na kazi kubwa iliyobaki ni kuhakikisha wanabaki na wanaishi milele

MECHI ZINAZOFUATA.
Liverpool Vs Manchester City   Anfield

Southampton Vs Wigan   St Marry's




0 comments:

Post a Comment