Alikuwa ni Marrouane Fellaini
na mchezaji bora wa mchezo wa jana aliyeharibu kabisa siku ya Sir Alex na
mashabiki wa Manchester Utd kote ulimwenguni baada ya goli lake kuipa Everton
na mashabiki wote pale marseysides sio tu point tatu bali pia zawadi ya
Idd.Inaweza kuwa mechi ya Manchester Utd na Everton ilyojaza mashabiki sio tu
kwenye uwanja wa Goodson Park bali pia hata hapa nyumbani kwetu Tanzania
kutokana na sababu kuu mbili.
KIUFUNDI
Manchester hawakuwa na mabeki wao
wote wa kati na pembeni wakianza na Valencia kulia pamoja na Karrick katikati na
kila mara inapotokea mpira wowote wa adhabu basi Nikica Jelavic na Marouane
Fellaine walionekana hatari.Bado walikuwa wanapata shida kupata muunganiko
mzuri wa Rooney ,Kagawa
MECHI INAYOFUATA.
Baada ya kupoteza mchezo wa jana
Manchester watakuwa Old Trafford Jumamosi wakiwakaribisha watoto wa Martin Jol
Fulham ambao wamenza ligi vizuri.Baada ya Van Persie kuanzia bechi leo Sir Alex
atakuwa na nafasi ya kumunzisha pamoja na Wayne Rooney ili waanze kutengeneza
uelewano na kuanza biashara ya kufunga magoli.Everton kwa upande wao watakuwa Villa Park kuwakabili Aston Villa na watatamani kuendeleza wimbi la ushindi walioupata jana.
KUMBUKA
Katika historia ya ligi kuu nchini uingereza ni timu moja tu ambayo mara mbili imeweza kupoteza mchezo wa ufunguzi na kuja kuchukua ubingwa.Na timu hiyo ni machester Utd msimu wa 1992-1993 na 1995-1996 kwa hiyo mashabiki wa Utd hawapaswi kupoteza tabasamu kutokana na matokeo ya jana.
0 comments:
Post a Comment