Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Wednesday, August 8, 2012

UWEKEZAJI MPYA AC MILAN


UWEKEZAJI MPYA AC MILAN
Akifanya ziara yake kwa mara ya kwanza nchini Urusi baada ya kipindi cha muda mrefu, hatimaye ziara ya aliyekuwa waziri mkuu na mmiliki wa klabu ya AC Milan Silvio Berlusconi imeonesha kuzaa matunda.Akiwa Urusi alimtembelea rafiki yake wa muda mrefu Vladimir Putin ambaye ndiye Rais wa nchi ya Urusi na kufanikiwa kuzungumza naye mambo kadha wa kadha ikiwepo kuomba uwekezaji wa makampuni na hata matajiri watakaoweza kuwekeza katika klabu ya AC Milan.
Tetesi zinasema kuwa tayari kampuni ya Gazprom iliyopo nchini Urusi ambayo inashughulika na uchimbaji wa gesi na mafuta imekubali kuwekeza katika klabu hiyo kwa kutoa mkwanja wa takribani hela za ulaya (euro mil 180) kwa kuanzia.Taarifa hizi zimetoka katika chombo kimoja cha habari nchini Hispania kinachojulikana kama AS ambacho kinataarifu pia serikali ya Urusi ndiyo wamiliki wa kampuni hiyo ya Gazprom tangu mwaka 1989.
Kampuni ya Gazprom ilianzishwa mwaka 1989 katika nchi iliyojulikana kama Soviet Union ambayo ilikuja kumeguka na kupatikana  nchi ya  Urusi.Ni kampuni inayomilikiwa kwa kiasi kikubwa na serikali ya Urusi kwa 50%.Kampuni hiyo inasadikiwa kuwa ina utajiri wa dola za kimarekani billion 44.6(US $44.6 bil).
Lakini kwa taaifa yako tu wewe mpenzi wa soka ni kuwa kampuni hiyo ya Gazprom ndiyo wadhamini wa klabu za Zenith St.Petersburg ya nchini Urusi pamoja na klabu ya Schalke 04 ya nchini Ujerumani.
Forza Milan kwa udhamini huo.

0 comments:

Post a Comment