Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Tuesday, August 7, 2012

NI KWELI USMANOV ANA DHAMIRA YA KURUDISHA MAKOMBE EMIRATES?


A

lisher Burkhanovich Usmanov huyu jamaa ni mtu hatari sana.Mtoto wa aliyekuwa jaji wa zamaniTashkent Burkhanovich Usamanov nchini Uzbekistan zamani Uzbekrussia.Ni mtu wa tatu kwa utajiri nchini Russia na anashika nafasi ya 28 ulimwengini mbele ya rafii yake kipenzi Roman Abromovic mmiliki wa timu ya Chelsea na kwa sasa akiwa anamiliki takribani 29% ya hisa zote katika timu ya Arsenal nyuma ya tajiri wa kimarekani Stan Kroenke akiwa na 60% lakini uatajiri wake kwa ujumla  unakadiriwa kuwa na kiasi cha paundi za kiingereza 19 billion.

Usmanov
Usmanov amezaliwa mnamo  tarehe 9/9/1953 huko nchini Ukraine  japo amekulia sana Uzbekistan kutokana na shughuili za kikazi za baba yake.Baadae akapata elimu yake katika chuo cha masuala ya mahusiano ya kimataifa kijulikanacho kama Moscow state institutes of international relations akihitimu katika shahada ya masuala ya sheria za kimataifa  na mnamo mwaka 1992 akavuta jiko akimuuoa bibi Irina Viner wa kabila la wajewish.

Ahitimu  shahada ya kwanza kwenye masuala ya mahusianao ya kimataifa.Usmanov Chuoni hapo alibobea na kukijkita zaidi kwenye sheria za kimataifa na baada ya hapo alianza kujihusisha na masuala ya biashara za kimataifa  akianza kutengeneza utajiri wake katika biashara ya kutengeneza mabegi ya plastiki na baadae kuibukia katika biashara ya vyuma akiwa na kampuini inayoitwa Mettaloinvestments ikimpatia umaarufu mkubwa ikimiliki makampuni kama Mikhalovisky Gok,Moldavia metal ,pamoja na Ormel,ogrsk iron ore company akimiliki 45% ya hisa yenye thamani ya #13bilions.

Usmanov amekuwa na nguvu sana mpaka  kwenye Duma na serikarini kwa ujumla. kutokana na utajiri wake na baba yake kufanya kazi kwenye mahakama ya Uzbekistan  zamani ikijulikana kama Uzbekrussia kwa mda mrefu amekuwa na urafiki na viongozi wa ngazi mbalimbali nchini Urussi na katika vipindi tofauti akiwasaidia hata baadhi kushika hatamu akiwemo waziri wa zamani  na Rais wa sasa wa Urussi Vladimir Puttin.Usmanov kurinda urafiki wake na Puttin alimfukuza mhariri wa moja ya magazeti yake akimtuhumu kuandika habari za uchochezi kumchafua.
Arsenal Miaka ya Mafanikio
.
Usmanov apigwa miaka sita jela 1980.Maisha yake tangu utotoni yaligubikwa na utata na utukutu mwingi  alilotaka yeye ndio aliolofanya hata kama lillihatarisha maisha yake .Kujihusisha kwake na makundi ya kijasusi na bishara haramu alijikuta akitiwa nguvuni kwenda kutumikia kifungo cha miaka sita jela. Lakini baadae aliachiliwa huru kutokana na Rais wa  wakati  huo Uzbekistan huo Kerimov kuwa na mahusiano mazuri na Rais wa kundi la kijasusi na kuuza madawa haramu  anayeitwa Rakimov ambaye pia alikuwa na mahusiano mazuri na binti wa Usmanov.

Usmanov na Arsenal anasema.”Arsenal ndio timu ya kwanza kuiona kwenye televisheni na nikaipenda” Na moja kwa moja nikatambulishwa kwa Arsenal legends Devid Dein na rafiki yangu na tangu hapo nikatamani sana kuwekeza katika tmu hii kwa sababu wakati ule nilikuwa natafuta timu ya kuwekeza kwenye ligi kuu ya Uingereza.

Anunua hisa Arsenal. Mnamo mwaka 2007 Devid Dein akamuuzia Usmanov hisa zake 14% chini ya kampuni ya RED and WHITES  na kuondoka kwenye bodi baada ya kutofautiana na viongozi wenzake.Baada ya kununua hisa Usmanov akampa shavu Dein kuwa mwenyekiti wa kampuni ya RED and WHITES.Lakini baadae watu wakahoji mapenzi yake na Arsenal kwamba ataitetea kampuni ambayo imenunua hisa na imeingia mkataba  na Arsenal  ambayo sasa yeye ndo mwenyekiti au Arsenal?  Mapenzi ya Dein na Arsenal sio  ya kujificha akiwa kiongozi zaidi ya miaka 20 kuona hivyo akaamua kuachia ngazi asiharibu uhusiano wake na mashabiki.Itaendelea……………………..

0 comments:

Post a Comment