Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Saturday, August 11, 2012

NGAO YA JAMII-NI MAN CITY DHIDI YA CHELSEA



NGAO YA JAMII



 NI MAN CITY DHIDI YA CHELSEA,TUTARAJIE NINI NGAO YA JAMII?
Ngao ya jamii ya chama cha soka nchini  Uingereza ni mechi ambayo hukutanisha mabingwa wa premier league na mabingwa wa FA katika uwanja utakaochaguliwa na chama cha FA nchini Uingereza.. Ni mechi ambayo kama bingwa wa ligi ikitokea akawa bingwa wa FA pia, timu iliyoshika nafasi ya pili kwenye ligi inapata fursa ya kushiriki katika mchezo huo na bingwa wa vikombe vy FA na Ligi kuu. Mara nyingi mechi hii inachukuliwa kama ya kirafiki iliyo na mvuto wa kipekee unaotumika zaidi kuonyesha wachezaji wapya wa timu shiriki na wakati huohuo timu iliyo chini kidogo ya ligi kuu na FA na kufahamika zaidi kama. Hii inathibitishwa na kauli aliyoitoa kocha wa Manchester united Sir Alex Furguson kabla ya mechi mwaka 2008 akisema “Siku zote hii ni mechi ambayo hatuchezi kufa na kupona, tunaitumia kama kipimo cha kikosi”
KWA NINI INAITWA NGAO YA JAMII?
Sababu kuu ya kuitwa ngao ya jamii ni mapato yatokanayo na mechi hii ambayo hugawiwa kwa taasisi za kijamii, mapato ya getini pamoja na mapato yanayotokana na mauzo ya haki zote za mechi hii husambazwa kwa vilabu 124 vilivyoshiriki katika kombe la FA kuanzia raundi ya kwanza na kuendelea kwa dhumuni kubwa la kusambaza katika ‘projects’ au miradi mbalimbali ya kijamii. Mechi ya kwanza ya ngao hii ilichezwa msimu wa  1908/09 ikiwakutanisha Manchester United kama bingwa wa ligi daraja la kwanza dhidi ya Queens Park Rangers kama bingwa wa Southern league ambapo Man U iliibuka na ushindi wa 4-0 baada ya mechi ya kwanza kuisha 1-1 ndani ya uwanja wa Stamford Bridge.
IMETOKEA WAPI?
Ngao ya jamii, wakati huo ngao ya hisani ilianza mwaka 1898/99 ikijulikana kama Sherriff of London Charity Shield ikwakutanisha wanataaluma (Proffessionals) na wasio na taaluma (Amateurs). Lengo kuu la hili ilikuwa ni kumkaribisha Sheriff mpya wa jiji la London. Mfumo mpya ulianza mwaka 1908 ukiwakutanisha bingwa wa ligi daraja la kwanza na wa Southern league (Man U Vs QPR).
Mfumo wa mashindano haya umeendelea kubadilika siku hadi siku: mwaka 1913 ilikuwa ni baina ya wanataaluma na wasio na taaluma, mwaka 1921 ilikuwa ni baina ya bingwa wa ligi na bingwa wa kombe la FA kwa mara ya kwanza. Mfumo huu uliendelea kubadilika mpaka miaka ya 1920 kwa Proffessionals na amateurs kukutana lakini mnamo mwaka 1930 mfumo wa bingwa wa ligi na wa kombe la FA ukarudi tena mpaka leo hii.
Add caption
Mnamo mwaka 1971, Arsenal ikawa ni timu ya pili kuchukua mara mbili mfululizo tokea lianzishwe na mwaka 1974 Katibu mkuu wa FA, Ted Croker akatengeneza mfumo mpya wa mechi zote kuchezwa katika uwanja wa Wembley ukijumuisha bingwa wa ligi kuu na bingwa wa FA Cup.
NINI MVUTO WA MECHI HII BASI
Mechi hii huashiria ufunguzi wa msimu mpya wa ligi na mashabiki hupata fursa ya kuona wachezaji wapya, jezi pamoja na mfumo mpya utakaotumiwa na timu zao, hivyo basi wadau wengi wa soka wakiwa wamekaa takriban miezi mitatu wanapata fursa ya kuangalia timu zao kwenye mashindano mbalimbali.
VIPI MSIMU HUU?
Kama utakuwa na kumbukumbu Manchester Utd ndiyo mabingwa watetezi wa ngao hii walioipata kwa kuwalaza wapinzani wao Manchester city 3-2 mnamo tarehe 7 agasti 2011. Mwaka huu tutapata fursa ya kushuhudia miamba miwili, Manchester city wakiwa mabingwa wa Ligi kuu ya Premier(EPL) dhidi ya Chelsea wakiwa mabingwa wa FA na UEFA champions league jumapili ya tarehe 12 mwezi huu wa nane katika uwanja wa Villa Park, jijini Birmingham. Manchester city inacheza ikiwa bila kuwa na usajili wowote mkubwa kama ilivyozoeleka  huku wengi wakiongelea suala la usajili kusinzia akiwamo kocha wao Roberto Manchini, pamoja na hilo bado kuna wachezaji wa kuogopwa kama Silva, Yaya Toure na  Aguero. Kwa upande wa pili mambo ni tofauti kidogo, naweza kudiriki kusema Chelsea ni timu yenye safu ya kiungo bora kabisa ligi kuu ikiwaunganisha wachezaji wapya kama Oscar, Marko Marin na Eden Hazard na wa zamani kama Malouda, Ramires, Lampard, Mikel na Essien. Nadhani utakua umepata picha ni jinsi gani mechi hii itakuwa na mvuto tofauti na miaka kadhaa iliyopita.
Mwaka huu wa 2012, Community Shield au ngao ya jamii itachezwa tofauti na Wembley na Millenium kwa sababu ya viwanja hivyo kutumika kwa mashindano ya Olympics. Kuna uwezekano mkubwa kwa mechi hii kupigwa katika viwanja vya Sports Direct Arena (Newcastle), lakini zaidi ni Villa Park huko Birmingham.









VIKOSI TARAJIO
Man City: Hart, Zabaleta, Clichy, Coates, Company, Yaya, Barry, Silva, Nasri, Tevez, Aguero
Chelsea: Cech, A.Cole, Luiz, Terry, Ivanivic, Mikel, Lampard, Marin, Ramires, Hazard, Torres
JE WAJUA?
·         Timu yenye mafanikio zaidi kwa mashindano haya ni Manchester United ikiwa imechukua mara 15 ikifuatiwa na Liverpool mara 10, Arsenal 12, Everton 9 na Spurs 7.
·         Mechi ilyotoa magoli mengi ni kati ya Manchester Utd iliyoifunga Swindon Town 8-4 mwaka 1911.
·         Everton inashikilia rekodi ya kushinda mfululizo (4) toka mwaka 1984-1987 na Man U inashikilia rekodi ya kuwa timu iliyocheza mara nyingi mfululizo kuanzia mwaka 1998-2001.
·         Pat Jennings (Spurs) ni kipa wa kwanza kufunga goli na akiwa katika eneo lake la penati dhidi ya Man U.
·          Leicester city na Brighton ni klabu pekee zilizochukua ngao hii bila kuwa mabingwa wa aidha ligi au FA cup.
IFUATAYO NI ORODHA YA TIMU ZILIZOFANIKIWA KUITWAA NGAO HII.
Manchester United       19
Liverpool                            15
Arsenal                                               12
Everton                                               9
Tottenham Hotspur       7
Chelsea                                               4
Wolves                                4
Manchester City              3
Leeds United                    2
Burnley                                               2
Ni nani ataibuka mbabe mwaka huu?jumapili ya tarehe 12 mwezi wa nane, Villa Park, Manchester City Vs Chelsea.

0 comments:

Post a Comment