
Ligi kuu ya soka nchini England imeendelea tena kwa mechi mbalimbali kupigwa katika viwanja mbalimbali huku macho ya wapenda kabumbu yakiwa zaidi katika viwanja vya DW uwanja unaomilikiwa na klabu ya Wigan pamoja na pale Etihad Stadium kunako jiji la Manchester.

Katika uwanja wa DW klabu ya Wigan iliikaribisha masheatani wekundu Man United.Katika pambano hilo kulikuwa na mandhari nzuri kwa kocha wa Man United Sir Alex Ferguson ambaye jana tarehe 31/12/2012 alitimiza umri wa miaka 71.Hongera sana kwa siku ya kuzaliwa Sir Alex Ferguson.Katika mechi hiyo Man United iliibuka na ushindi wa magoli 4-0 huku shukrani ziwaendee washambuliaji wa Man United Javier Hernandes 'Chicharito' aliyefunga magoli 2 na Robin Van Persie kufunga magoli 2 pia.
0 comments:
Post a Comment