Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Monday, December 3, 2012

ARSENE BADO ATALITETEA KOMBE LA ARSENAL


Arsene Wenger

 Usicheke hiyo ndio hali halisi kwani sio  tangu kuanza kwa msimu huu na wa jana wala wajuzi na sasa ni kwaida sana.Historia inasema mwaka 1998 Arsenal baada ya michezo 15 walikuwa na point 4 zaidi ya za leo nab ado waliweza kuishika nafasi ya pili kwa hiyo bado wana nafasi kubwa ya kutetea kombe lao kama kawaida.Kwa kuziangalia takwimu hizi huwezi kuuliza kwamba kwa nini wachezaji hawajitumi kwani ni ukweli  usiopingika kwamba Poldoski na hata Santi Carzola wameshapewa mwongozo wa kazi na kile ambacho mwisho wa msimu bosi anataraji kutoka kwao.Hivi jiulize Swali dogo tu ni kwenye timu gani ya Premier  waweza kuupata muunganiko huu wa Arteta,Carzola na Wilshere jibu ni rahisi tu hakuna lakini kwasababu anajua atakachoulizwa mwisho wa msimu hawezi kujitoa kwa tone lao la mwisho.Ni ukweli usiopingika kwamba Arsenal kwa sasa hawanufaiki na uwezo wa mwisho wa wachezaji wao na tatizo ni wimbo ule ule ubinafsi wa Wenger na bodi yake.

Arsenal ni timu ambayo inategemea sana uimara wa sehemu ya kiungo kutokana na mfumo ambao timu inatumia wa 4-3-4 au 4-5-1.Kiungo ya Asrenal bado haijaiva na kuelewana vya kutosha na hatimaye kupiga pasi za haraka na kutengeneza nafasi za kutosha matokeo yake kwa asilimia kubwa ya mchezo mtu ambaye ameachwa mbele anakuwa ametengwa kwa mda wote wa mchezo. Kwa sasa mfumo wa 4-4-1-1 ungeweza sana kuisaidii timu kwa kuwa na ama Carzola na Walcott pembeni, Gervinho bado hawezi kuwa mchezaji Wenger  anamtegemea hata kidogo. Katikati Jack Wilshere na Arteta halafu mbele awepo Poldoski na Giroud mfumo huu sio tu unatukumbusha The Invicibles lakini pia utaleta balansi ya timu kwa hali ya sasa.
 We meet again: Arsenal will travel to Swansea
Mzee Ferguson amekuwa mjanja sana katika eneo hili msimu ulipoanza akianza na mfumo wa 4-2-3-1 mfumo huu nao kwa kiasi kikubwa unahitaji uimara wa sehemu ya kiungo sehemu ambayo United hawako vizuri sana hasa mfumo huo ukimtegemea sana Shinji Kagawa aliyepata majeraha.Kilichofanyika baadae akarudia mfumo wake wa kila siku wa 4-4-2 huu ukitegemea sana Winga sehemu ambayo pia United wako vizuri  huku akiendelea kupata matokeo lakini pia akisubiri kiungo yake kuimarika na kuutumia mfumo  anaokusudia.

Hakika mawazo ya watawala hapa sio ya mashabiki wala wachezaji utamskia mwenyekiti Peter Hill-Wood akikumabia baada ya miaka miwili Arsenal itakuwa moto wa kuotea mbali je wachezaji nyota wataweza kuvumilia? Au watafuta nyayo za wenzao walioshindwa kuvumilia? Kwa  kweli kama unataka uendeleee kufurahia maisha na wenzako usiwe na matarajio makubwa sana na Arsenal kwa sasa unatakiwa uishi kama bodi ya Arsenal na mzee Wenger wanavyotaka kwa sasa kwani hakikia watalitetea kombe lao.

0 comments:

Post a Comment