Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Thursday, October 18, 2012

WILSHERE: NIKO TAYARI KWA MAPAMBANO


Getting a run: Jack Wilshere played 90 minutes for Arsenal in a friendly defeat to Chelsea

















Kiungo wa kutumainiwa wa Arsenal na timu ya taifa ya Uingereza  Jack Wilshere amemweleza kocha wake Arsene wenger kwamba baada ya kuwa nje ya uwanja kwa takribani miezi 15 sasa yuko tayari kupambana.Wilshere jana alicheza dhidi ya Chelsea kwa dakika tisini kwa mara ya kwanza tangu aumie mwezi wa nane msimu uliopita huku Arsenal wakipoteza mchezo huo kwa 2-0.Kumbuka mchezo wenyewe ulihusisha vikosi vya chini ya umri wa miaka 21 lakini pia kwa nyakati tofauti makocha hutumia hata wachezaji wao wazoefu hasa wanapotoka katika majeraha.Achilia mbali mchezo wa jana Wilshere pia tayari ameshacheza kwa dakika 136 katika michezo dhdi ya Westbromwich Albion pamoja na Reading na sasa anasema yuko tayari hata kuwavaa Norwich jumamosi pale Carow Road.Lakini tayari Wenger alishasema wazi kwamba lazima waende taratibu taratibu japo kipaji na uwezo wa Wilshere unaweza ukamtia majaribuni kocha yeyote na kujikuta ukimtumia pasipo kupenda lakini yeye anasema atayashinda.Jopo la madaktari na Wenger  wamempamgia mchezo mwingine wa kujipima nguvu dhidi ya Everton japo anaweza kuwepo hata benchi katika mchezo dhidi ya Norwich na ule wa klabu bingwa Ulaya dhidi ya Schalke 04.Mchezo wa Capital League One  dhidi ya Reading mwishoni mwa mwezi huu ndio yawezekana ikawa ndio tarehe yenye uhakika zaidi ya hatimaye Wilshere kurejea kunako kikosi  cha kwanza cha washika mitutu hao wa pale Emirates.
 Target: Midfielder Wilshere could be back in the Arsenal first team by the end of October

0 comments:

Post a Comment