Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Monday, October 22, 2012

WAYNE ROONEY NI MANCHESTER UNITED NA MANCHESTER UNITED NI WAYNE ROONEY




Wayne RooneyRemember the name: Rooney celebrates his winner for Everton against Arsenal in 2002
Unajua kupigana mtaani? Asikudanganye mtu ngumi za mtaaani ni ngumu sana tofauti na za ulingoni ambazo sheria zaidi imezitawala katika kumpata mshindi.Hata nakumbuka Dareck Chisola alishinda kwenye ngumi za mtaani wakati ametoka  kuchakazwa na Vitali Kitschiko wakapishana  maneno na  David Haye na baadae kurushiana makonde mbele ya waandishi wa habari lakini walipokuja ulingoni  hakufua dafu alichakazwa vibaya sana. Unajua ni kwa nini kwasabau ngumi za mtaani hazina mpangilio unacheza vile utakavyoona itakusadia kushinda pambano na huyu ndiye Wayne Mark Rooney  maarufu kama Wazza.Alipoulizwa kuhusu kipaji cha Rooney wakati alipoifungia Everton mabao nane katika michezo nane kwenye michuano ya vijana mtafuta vipaji wa Everton Bob Pandleton ambaye ndiye aliyemleta Everton akiwa na umri wa miaka 9 tu anasema he is a street Fighter.

Mwongo mmoja katika ligi kuu ya premier pale uingereza akiwa na umri wa miaka 26 ni kitu kikubwa sana na tayari ameshashinda karibu kila kitu kwa United.Makombe manne ya ligi kuu ya premier Uingereza,amecheza fainali tatu za klabu bingwa barani Ulaya na kuchukua moja ni kielelezo cha kutosha kuonyesha ni mchezaji wa aina gani.Roho yake ya kipambanaji inabeba dhana nzima ya Manchester United na ndio maana  hata kibabu Fergie anaonekana hafurukuti hapa.Hebu fikiria ni Ferguson yupi unamwambia eti hapa hakuna mchezaji wa kariba yangu hapa united? hebu muulize Roy Keane kilichomtokea baada ya kauli kama hii lakini Rooney ameambulia kuongezwa mshahara na kufanywa mchezaji ghali kuliko wote Uingereza.Pale Old traford wamepita watu kama Cristiano Ronaldo,Roy Keane kina David Beckham wakionekana kama ndio nembo ya soka sio kwa United pekee lakini hata Uingereza kwa ujumla waliondoka vibaya lakini sio Rooney. Hatari huyu mtu achiila mbali kwamba anataka kuonekana mshindi wakati wote lakini pia hajali mbinu anayotumia kushinda ndio maana kadi nyekundu na Rooney ni wamekuwa ni marafiki walioshibana kweli kweli
 Says it all: Rooney jokes with Manchester United manager Sir Alex Ferguson

Watu wanasema eti babu Fergie kapunguza ukali siku hizi lakini mimi naona sio kweli hivi katika ulimwengu huu wa soka utampata wapi sio Wayne Rooney tu lakini nyota anayelipwa 250,0000 kwa juma halafu yuko tayari kucheza namba yoyote uwanjani? Amini usiamni leo hata  Ronaldo na Messi wasajiliwe United huwezi kukosa nafasi ya Rooney uwanjani. Wakati kama huu ambao sehemu ya kiungo ya Uinited haina ubora sana utamuona sana Rooney akifanya ya Carrick na Scholes halafu wanapata matokeo huyu jamaa ni tarajio la kila kocha. Mwenyewe anasema anataka kumaliza soka yake akiwa kama mchezaji wa sehemu ya kiungo na hakika kwenye upigaji wa pasi sahihi kwa wakati sahihi ni eneo ambalo limeongezeka sana ubora kwa Rooney.Wakati Fulani Jose Mourinho aliposikia Rooney katangaza anataka kuondoka United unakumbuka alichokisema?” Eti sina hakika sana kama ni kweli ila kama ni kweli nimeacha simu yangu  wazi Ferguson anipigie” Unakumbuka lile goli la takribani mita 30  alilowafunga Arsenal ni goli lake la kwanza ligi kuu ya premier pale uingereza wakati ule yuko Everton? Unajua Wenger alisema nini?” Kwa miaka  aliyokuwa nayo hakuna muingereza mwenye kipaji kikubwa cha kwake hakika ni hazina kwa miaka mingi inayokuja”

 Ready for responsibility: Wayne Rooney wearing the captain's armband
Kwa wale waumini wa takwimu Rooney tayari ameshatupia nyavuni magoli 181 katika michezo 371 aliyoichezea United na kwa uwiano tayari anawaacha nyuma magwiji kama Sir Bobby Chalton,George Best,Andy Cole pamoja na kocha wa sasa QPR Mark Hughes. Msimu uliopita amefunga jumla ya magoli 34 na kusajiliwa kwa Van Persie tayari kumeibua maswali na minongo’no  kwamba je atakubali kutoka eneo la ufungaji lakini Rooney tayari ameshaanza kuonyesha kwa Van Persie kile kile allichokionyesha kwa Cristiano Ronaldo miaka mitatu iliyopita.Hivi  majuzi aliiongoza Uingereza katika mchezo wa kufuzu fainali za kombe la duinia dhidi ya Poland akichukua nafasi ya Steven Gerrard aliyekuwa anatumikaia Adhabu ya kadi. Na tayari mijadala mingi imeibuka kwa je Rooney anatosha kuwa nahodha wa Uingereza? Dhambi ya utovu wa nidhamu inamtafunaikisemekana ni mtu wa vimwana sana, mvuta bangi na hata akishutumiwa kucheza kamali na yale ya John Terry hayatasahaulika kirahisi kwene vichwa vya Wangereza na kubwa kabisa ni lile la kutoifungia timu yake  ya taifa goli  hata moja katika fainali za kombe la dunia na labda Brazil imekuja wakati muafaka kwake.













0 comments:

Post a Comment