Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Saturday, October 6, 2012

PREVIEW: WEST HAM VS ARSENAL




 Saving the best until last? West Ham host Arsenal in a London derby to conclude Saturday's fixtures

 Arsenal baada ya kupoteza mchezo wao kwa wa wapinzani wao wa jiji la London msimu huu dhidi ya Chelsea katika uwanja Emirates wanataka kujirejesha katika nafasi ya kuhesabiwa kama mabingwa ifikapo mwezi wa tano mwaka huu. Mchezo dhidi ya West Ham ni mchezo wa pili katika michezo mitano ambayo Arsenal itacheza msimu huu dhidi ya wapinzani wake wa jiji la London.Mchezo huu unaahidi kuwa mgumu kweli kweli achilia mbali ukweli kwamba West Ham  nao wanatoka  London pia  wanashika nafasi 7 na pointi zake 11 na Arsenal nafasi ya 8 na pointi zake 9 lakini mchezo wa Arsenal dhidi ya kocha wa West Ham Big Sam haukuwahi kuwa rahisi wakishinda mechi 2 tu katika mechi 9.

 Back with a bang: Andy Carroll performed well after coming off the bench in West Ham's 2-1 win at QPR on Monday
West Ham  wamenza vizuri ligi  msimu huu sio vizuri  kuliko Arsenal pekee bali kuliko timu zote ambazo zimepata nafasi ya kushiriki ligi kuu ya premier nchini Uingereza msimu huu.Aina ya mchezo wa West Ham na Sam Allardyce’s ni michezo ile ile ya wakina Stoke City na mbinu ambayo inahitahi watu wenye nguvu juu na chini na mbinu ambayo haimpi shida  Arsenal peke yake bali timu nyingi ligi kuu ya premier pale Uingereza. Na ni mbinu hii ndio imewahakikishia Stoke City maisha marefu ligi kuu ya Premier pale Uingereza tangu wamepanada  na hakika wataendelea kuishi milele na naona  West Ham wanataka kupita njia hii.
 Back in the game: Lukas Podolski levels for Arsenal
Lakini mchezo huu ni mchezo ambao Arsenal kwa kiasi  kikibwa inatarajiwa kuibuka na ushindi hasa baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Chelsea lakini pia mchezo dhdi ya Olimpiacos ambao arsenal iliibuka na ushindi wa 3-1 umeweza kuwarudisha Arsenal katika hali ya kawaida kisaikolojia na kuondoa hofu hasa kwa mabeki Thomas Vermaleen na Laurent Koscielny.

Kevin Nolan amekuwa anaiongoza West Ham kwa mfano mpaka sasa kwana anauwezo mkubwa wa kuituliza timu pale inapohitaji na  Ricardo Vaz te hakika amekuwa akifanya kazi ya kuvutia na kutoa ubunifu West Ham inaohitaji hasa akicheza nyuma ya Carton Cole au Andy Carroll.
 Influential: Gervinho hit two and was at the heart of much of Arsenal's attacking guile

Mzee wenger anasema ni kawaida kwa Arsenal kuwabadilisha wachezaji wa pembeni kuwa wachezaji wa kati kama alivyofanya kwa Thiery Henry na Robin Van Persie na sasa kawa Gervinho na Walcott ila atanishangaza sana kama atamtumia Gervinho katikati leo hasa kutokana na aina ya mchezo wa West Ham wanaoucheza ambao unahitaji nguvu zaidi.
 First up: Mohamed Diame fouled Shaun Wright-Phillips and picked up a booking

Sehemu ya kiungo ni sehemu muhimu sana kwa upande wa Arsenal hasa kutokana na aina ya mchezo waocheza wa pasi fupi na za haraka ukijulikana hasa kama mpira Wenger na wanabahati sana mpaka sasa kwamba baada ya kuwepo kwa wasi wasi kukosekana kwa Mikel Artea dhidi ya Olimpiacos katikati ya wiki lakini yuko fiti.

 Good feeling: Podolski is mobbed after his goal

 UKWELI KUULEKEA MCHEZO HUU

Achilia mbali ukweli kwamba Arsenal ndio wafalme wa London lakini mpaka sasa West Ham wameshinda mechi zote dhidi ya wapinzani wake jijini London wakishinda mechi dhidi ya Fulham na QPR.

Japo West Ham hawajapoteza mchezo wowote katika mji  wa London lakini pia usisahau kwamba hawajawahi kuifunga Arsenal tangu 2007.

Baada ya kuona hizi takwimu nilizitegemea sana kutokana na mchezo wanaocheza kwani West Ham ndio timu iliyopata kadi nyingi 15 kuliko timu yoyote katika  premier Ligi ya Uingereza.

Arsenal wanajivunia ukuta mzuri katika ligi mkuu mpaka sasa wakiwa wamefungwa goli moja tu mpaka sasa.

Kama Arsenal wataibuka na ushindi katika mchezo wa leo utakuwa ni ushindi wa 350 tangu Arsenal Wenger ateuliwe kuwa kocha wa Arsenal.
Vikosi vyaweza kuwa hivi.
WEST HAM
Jaaskelainen
Demel, Tomkins, Collins, Taylor
Noble, Diame
Vaz Te, Nolan, Jarvis na
Carroll
ARSENAL
Mannone
Jenkinson, Mertesacker, Vermaelen, Gibbs

Arteta, Ramsey, Cazorla, Podolski
Gervinho na Giroud













0 comments:

Post a Comment