
Hakika ni
jumapili nzuri sana leo kwa ndugu zangu wapenda kandanda kwani baada ya kutoka
katika nyumba za ibada kwa wale wakristu na kwa waislamu najua ibada pia
zinaendelea kama kawaida watu watakuwa wapo majumbani wakisubiria kwa hamu
mechi za leo.Leo naweza kuiita ni ‘Super Sunday’kwani kuna takribani mechi 3
mpaka 4 za kuzitazama likiwemo pambano la kukata na shoka kati ya Fc Barcelona
na Real Madrid katika dimba la Camp Nou pale nchini Hispania.
Kwa wale
mashabiki wa Ligi Kuu ya soka nchini Italia watapata kulishuhudia pambano la
kukata na shoka kati ya AC Milan dhidi ya Inter Milan pambano likijulikana kama
‘Derby Della Madoninna’.Lakini kwa leo ningependa nilizungumzie zaidi pambano
la watani wa jadi nchini Hispania maarufu kama ‘EL CLASSICO kati ya Barcelona
dhidi ya Real Madrid’.

Watu wengi
wanajiuliza kwa nini pambano hili linaitwa ‘EL Classico’.Jina la EL Classico
halikuanza zamani sana kwani lilianza katika miaka ya 2000.Asili yake ni katika
nchi za Amerika ya Kusini kutokana na kuongezeka nguvu kwa soka la Hispania
katika bara hilo la Amerika.Nchini Argentina pambano la wapinzani wa jadi kati
ya Boca Juniors na River Plate linajulikana kama Superclassico,wakati nchini
Mexico pambano la watani kati ya Club America na Guadalajara linajulikana kama
El Super Clasico.
Kabla hata
ya jina hilo la El Classico nchini Hispania,tayari mashabiki wa soka wa
Hispania walishaonja utamu wa upinzani wa jadi baina ya timu hizo tangu
mwanzoni mwa karne ya 20.Na moja ya sababu ya upinzani huu ni kuwa timu zote
mbili zimetoka katika majiji makubwa mawili nchini Hispania ya Madrid na
Catalunya.
Inasemekana
kuwa klabu ya Real Madrid inapendwa sana na viongozi wakubwa wa serikali pamoja
na familia ya kifalme ya nchini Hispania
huku watu wa jimbo la Catalunya ambapo klabu ya Barcelona ndipo inapotoka
inawakilishwa na watu wa kawaida na wenye kipato cha kawaida.Upinzani wa vilabu
hivi ulikolezwa zaidi na nguli wa soka duniani Alfredo Di Stefano ambaye amepewa
cheo cha Rais wa Maisha wa klabu ya Real Madrid katika miaka ya 1950 wakati klabu
zote mbili za Madrid na Bracelona zikiingia katika mgogoro wa kumsajili nyota huyo
aliyekuwa akikipiga katika klabu ya Derpotivo
Los Milonarios ya nchini Colombia.
Di Sefano
alivitoa udenda vilabu vya Real Madrid na Barcelona wakati akiichezea klabu ya
Deportivo Los Milonarios ya Bogota nchini Colombia.Alivyotoka Depo ya nchini
Colombia alijiunga na klabu ya River Plate ya nchini Argentina kabla ya vilabu vya
Barca na Madrid kila moja kumsajili na hivyo kuibua mgogoro mkubwa wa kuwa ni
klabu gani ilipaswa kupata sahihi ya mchezaji huyo.Mgogoro huo uliingiliwa kati
na chama cha soka cha nchini Hispania na kumuidhinisha Di Stefano kuichezea
klabu ya Real Madrid na Barcelona ikipigwa chini.
Katika
kuonesha yeye ni mchezaji hatari,Di Stefano alifunga magoli mawili mazuri
katika pambano la wapinzani hao wa jadi katika mechi yake ya kwanza dhidi ya
timu ya Barcelona wakati akiwa na jezi za Real Madrid.Upinzani wa jadi wa
vilabu hivi uliongezeka maradufu wakati timu hizo zilipokutana mara mbili katika
michuano ya Ulaya kati miaka ya 1960 na 1961.Mwaka 1960 Real Madrid iliifunga
klabu ya Barcelona katika fainali ya michuano hiyo ya Ulaya kwa sasa klabu
bingwa Ulaya na mwaka 1961 Barcelona
ilifanya vivyo hivyo.
Sababu
nyingine ya mechi hii kuwa na mvuto ni kitendo cha wachezaji nyota kuvichezea
vilabu hivi viwili katika nyakati tofauti.Wengi watakumbuka mwaka 1980 ambapo
wachezaji nyota Bernd Schuster alipoikacha Barcelona na kujiunga na Real Madrid
huku Michael Laudrup ambaye kwa sasa
anaifundisha klabu ya Swansea City ya nchini Uingereza akifanya hivyo mwaka
1990.
Mwaka 2000
Luis Figo akifanya vivyo hivyo kwa kuikacha Barcelona na kujiunga na klabu ya
Real Madrid.Pambano la kwanza baina ya timu hizi mbili lilifanyika tarehe 17
mwezi wa pili(Februari) mwaka 1929 pale Camp Nou huku Madrid ikiibuka na
ushindi wa magoli 2-1.Wakati uhamisho wa wachezaji kama Luis Enrique kutoka
Real madrid kwenda Barcelona na Luis Figo kutoka Barcelona kwenda Real madrid
ukizua vurugu kubwa lakini upinzani wa vilabu hivyo haujavizuia vilabu hivyo
kuuziana wachezaji.
Wachezaji
Ricardo Zamora,Josep Samitier,Bernd Schuster,Michael Laudrup na Ronaldo Di Lima
wote wamewahi kuvichezea vilabu hivi kwa nyakati tofauti.
Mechi ya
Leo.
Pambano la
leo kati ya Barcelona na Real Madrid linasubiriwa kwa hamu sana na wapenda
kabumbu takribani 400 duniani litakuwa la kukata na shoka.Barcelona wataingia
uwanjani huku wakiwa na listi ya majeruhi kama nahodha Carles Puyol
aliyevunjika mkono,Thiago Alcantara na kukiwa na hatihati kwa beki wake tegemeo
Gerad Pique kuwemo katika kikosi.Tayari viungo Alex Song na Javier mascherano
wametayarishwa kucheza ktika nafasi za mabeki wa kati kwa upande wa Barca.
Kwa Upande
wa Real Madrid mtihani mkubwa kwa kocha Mourinho utakuwa ni nani atacheza kama
kiungo mshambuliaji katika mechi ya leo kati ya Mesut Ozil,Luka Modric na
Ricardo Kaka.Na kati ya Essien na Sami Khedira nani kuanza sambamba na Xabi
Alonso katika kiungo.
·
Leo
ni mechi ya 222 kati ya wapinzani hawa wa jadi na kati ya hizo barcelona
kashinda mara 87 huku Real akishinda mara 88.
·
Ronaldo
kafunga magoli 12 katika mashindano yote magoli 2 mbele ya Lionel Messi mwenye
magoli 10.
·
Real
Mdrid imeshinda mara moja tu katika mechi 8 ilizocheza Camp Nou chini ya
Mourinho huku ikitoka sare mechi 1 na kupoteza 6.
VIKOSI TARAJIWA.
BARCELONA
Valdes
Alves, Song, Mascherano, Adriano
Xavi, Busquets, Iniesta
Pedro, Messi, Sanchez
Alves, Song, Mascherano, Adriano
Xavi, Busquets, Iniesta
Pedro, Messi, Sanchez
REAL
MADRID
Casillas
Arbeloa, Pepe, Ramos, Marcelo
Khedira, Alonso
Di Maria, Ozil, Ronaldo
Benzema
Casillas
Arbeloa, Pepe, Ramos, Marcelo
Khedira, Alonso
Di Maria, Ozil, Ronaldo
Benzema
0 comments:
Post a Comment