Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Monday, September 17, 2012

ULE USIKU WA ULAYA UMERUDI.




 KUNDINDI A.
 
 GNK  Dinamo Zagreb VS FC Porto
Paris Saint Germain vs FC Dynamo Kyiv.
Dinamo Zagreb na Fc Porto wameshakutama mara 4 katika michuano hii na mara zote Dinamo Zagreb ikichomoza na ushindi na mara ya mwisho walikutana kwenye msimu wa 1998/1999.

Paris Saint Germain na Dynamo Kyiv walikutana kwa mara kwanza kwenye michuanao hii msimu wa 1994/95 wakati huo golikipa wa Dynamo Kyiv Olexandr ShovkovSkiy akiwa na umri wa miaka 19 tu lakini kwa sasa akiwa na umri wa miaka 37 akicheza mechi zote. Lakini mara mwisho walikutana kwenye robo fainali ya michuano hii msimu wa 2008/09.

KUNDI B.
 Slow start: Giroud is yet to score for Arsenal
Montipellier VS Arsenal FC.
Olympiacos FC vs FC Schalke O4.
Ni  kipindi cha miezi mitatu tu tangu aondoke Stade dela Mosson  na kujiunga na Arsenal lakini michuano ya UEFA Champions League inamrudisha Olivier Giroud nyumbani haraka kuliko alivyotarajia.Ufaransa ni kama nyumbani kwa Arsenal hasa kutokana na ukweli kwamba sio tu ina wachezaji 7 wenye uzoefu wa ligi ya Ufaransa lakini pia ina wachezaji 6 ambao ni wazawa bila kumsahau kocha Arsene Wenger.

Beki wa kati wa Schalke 04 Mgiriki Kyriakos Papodopolous ameiwakilisha Olympiacos katika michuano msimu wa 2007/10.Olympiacos imecheza michezo 6 ya kuishindani na timu kutoka Bundesliga na yamefungwa magoli 29 katika michuano hiyo ya Ulaya.

KUNDI C.
 Kevin Prince Boateng in AC Milan-Sampdora
Malaga CF vs Zenit St Petersburg
AC Milan vs RSC Anderlecht.
Malaga wameshafungwa magoli 3 tu katika michezo 9 waliyocheza nyumbani kwenye mashindano haya ya Ulaya.Zenit kwa upande wao wameshatembelea Hispania kwenye michuano hii mara 4 na wakipoteza michezo 4.

Milan kwa upande wao wanafurahia sio tu kuanza michuano hii nyumbani lakini pia kucheza na Anderlecht kwani mara mbili walipokutana Milan alifanikiwa kushinda na baadae kwenda kuchukua kombe.Japo kocha Allegri anakabiriana na kibarua kigumu kwa mashabiki pale San Siro kwani wameanza vibaya Serie A hasa michezo ya nyumbani ambako hakujawahi kuonekana zaidi ya miaka 80. Anderlecht kwa upande wao wametembelea Italia mara 14 katika michuano hii na hawajapata ushindi hata mchezo1.

KUNDI D.
 Row: Ronaldo and Jose Mourinho
Borrusia Dortmund vs AFC Ajax
Real Madrid CF vs Manchester City FC.
Borrusia Dortmund imekutana mara 4 na timu za Uholanzi katika michuano na hakufanikiwa kupata ushindi mara zote .Kocha wa sasa  wa Ajax Frank de Boer alikuwa kwenye kikosi ambacho kiliifunga Dortmund kwenye robo fainali ya michuano msimu wa 1995/96.

Cristiano Ronaldo alipokuwa mchezaji wa Manchester United ameshakutana na Manchester City katika kile kinachojulikana kama Manchester derby mara 11 na akifanikiwa kutoka na ushindi mara 7 na kupoteza mara 3.
JUMATANO.
KUNDI EThe snub: Anton Ferdinand ignores John Terry's handshake

FC  Shakhtar vs FC Nordsjaelland.
Chelsea FC vs Juventus.
Sakhtar na Nordsjaelland hawajawahi kukutana katika mechi yoyote ya kimashindano lakini wamekutana 2011 katika mchezo wa kirafiki na mabingwa hawa wa Ukraine Nordsjaelland wakishinda kwa 3-1.

Juventus imesafiri mara 18 kwenda Uingereza na katika mara zote kibibi kizee cha Turin kimefanikiwa kupata ushindi mara 2 tu.Chelsea kwa upande wao kwenye ile safari yao kwenda kuchukua Ubingwa wa mashindano haya msimu uliopita aliifunga Napoli kutoka Italia .

KUNDI F.
 Germany: Bayern Munich - FSV Mainz 05, Bastian Schweinsteiger celebrates
LOSC Lille vs FC  BATE Borisov.
FC Bayern Munich vs Valencia CF.
BATE na Lille wote kwa pamoja wamepata wakati mgumu sana kufika hatua ya makundi.Lille walihitaji mpaka muda wa nyongeza kuitoa FC Kobenhvn katika mchezo wa mtoano.BATE nao mabingwa hawa wa Belarus nao walihitaji mpaka muda wa nyongeza kuwafunga FC Vardar magoli 2 kufika hatua ya makundi.

Bayern vs Valencia inatukumbusha fainali ya mwaka 2001 fainali ambayo Bayern walishinda kwa njia mikwaju ya penati.

KUNDI G.
 Not so mellow yellow: Cesc Fabregas is ready to fight for his place at Barcelona
FC Barcelona vs FC Spatark Moskva.
Celtic FC vs SL Benfika.
Mchezo huu utashuhudia kocha wa  sasa wa Barcelona TItto Vilanova akiiongoza timu hiyo kwa mara ya kwanza katika michuano hii akiwa kama kocha mkuu.Kocha wa Spartak Mhispania Unai Emery atakuwa anasaka ushindi wake wa kwanza dhidi ya Barcelona akifanya hivyo mara 13 bila mafanikio.

Celtic ameshakutana na Benfica mara 2 katika mashindano haya na mara zote walifanikiwa kufika hatua ya makundi.

KUNDI H.
 Timeless: Paul Scholes continues to defy the years, scoring the first in another sensational display against Wigan
Manchester United FC vs Galatasaray AS.
SC Braga vs CFR 1907 Cluj.

Kwa mara ya kwanza Garatasaray walitembelea Old Traford ilikuwa ni msimu wa 1993/94 katika mchezo ambao uliisha kwa sare ya 3-3 na hata hivyo hawajawahi kupata ushindi Old Trafford.

Braga na CFR hawajawahi kukutana katika michuano hii japo CFR wana wachezaji 6 kutoka Ureno wakiwemo 3 kutoka Braga.














0 comments:

Post a Comment