Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Saturday, September 29, 2012

PREVIEW: ARSENAL VS CHELSEA




 La London derby: Spaniards Santi Cazorla and Fernando Torres go head-to-head

 Ni moja kati ya wiki muhimu sana kwa Arsenal baada ya wiki iliyopita kuwalazimisha mabingwa watetezi Manchester City sare pale Etihad wiki hii watakuwa Emirates kuwakaribisha  watani wao wa jijini London Chelsea na pengine ni wakati mzuri  kumuonyesha kila mtu kwamba wako tayari kwa mbio  za ubingwa msimu huu hawatanii.Mechi yenyewe inaahidi kuwa mechi nzuri na ya kusisimua pengine kuliko msimu uliopita achilia mbali utani wao jijini London lakini Chelsea msimu wako tofauti kutokana na aina ya wachezaji iliyowasajili

Chelsea wanaweza wakawa wameshinda ile vita ya nani ni mfalme na fahari ya jiji la London kwa kuchukua UEFA Champions league msimu uliopita lakini kitu pekee kinachomsumbua na kumtoa mate mmiliki wa Chelsea Roman Abramovic ni mpira Wenger. Mpira Wenger umemlazimisha Abramovic kufungua pochi na kuwaleta Eden Hazard,Marko Marin,Oscar the new Kaka’ na japo Marin bado hajacheza lakini tayari hao waili wameshaonyesha thamani zao kwa muda mchache.

Didier Drogba vs Arsenal.
 Missing man: Didier Drogba is at Shanghai Shenhua now
Arsenal na Arsene Wenger hatimaye watakuwa na tabasamu kuelekea huu mchezo kwani hatimaye wanaenda kukutana na Chelsea bila Didier Drogba.Tembo huyu ameshawakosesha sana usingizi mashabiki wa Arsenal kwani anaweza kwa msimu huo akawa amepoteza ubora wake lakini mechi dhdi ya Arsenal ikamrudisha.Takwimu zinaonyesha katika michezo 14 aliyocheza dhidi ya Arsenal hajafunga mchezo 1 akifunga michezo 13 ikiwa ni  wastani wa goli 1 kila mchezo hakika Chelsea watamkosa mtum huyu.Drogba ameenda zake Shaghai Shenshua bure na Wenger  anasema nadhani Chelsea wanammisi sana ila sio Arsenal emeshatuumiza sana akikieleza kituo cha Sky sports. Takwimu nyingine zinaonesha Drogba akiwa Chelsea Dhidi ya Arsenal W7,D3,L1 na bila ya Drogba W0,D9,L13 je leo itakuwaaje?

MIPAMBANO MUHIMU LEO.

Eden Hazard vs Karl Jenkison.
 Breakthrough: Jenkinson has established himself in the Arsenal first team
Hakuna shaka kwamba beki huyu wa kulia wa Arsenal Karl Jenkison anaendelea kuimarika siku hadi siku na kuwafanya mashabiki wa Arsenal wasahau kwamaba kuna mtu anaitwa Bacary Sagna na moja kati ya sehemu ambazo Wenger atakuwa na wakati mgumu msimu huu.Mechi 5 zilopita inawezekana amekutana na watu wasumbufu ila sio Eden Hazard  Eden =” the bibilical place which has got natural talents and Wonders”) Hazard = Dangerous = Hatari  na jina la kitabu linasadifu yaliyomo.

Wenger vs Walcott.
 Staying put: Walcott wants to pen a new deal with the Gunners
Achilia mbali kwamba kuna matatizo ya mktaba ambapo Walcott mwenyewe amesemea atasaini hivi karibuni kwani anataka afanye yale ambayo yamefanywa na mtu ambaye anavaa jezi yake na huyu sio mwingine ni Thiery Henry.Wacott anaonekana kazi anaiweza achilia mbali kasi yake  na umaliziaje wake ambao unaimarika siku hadi siku lakini hata takwimu zake dhidi ya  Chelsea mimi nampa nafasi ya kuanza mbele ya Gervnho.Walcott ameendelea kusisistiza kwamba anataka kucheza kama mshambuliaji wa kati na Wenger mwenyewe anasema binafsi anamuona kama mshambuliaji wa kati lakini inabidi awe mstahimilivu kidogo.

David Luiz vs Giroud.
 Worth fighting over: John Terry holds off Jonathan Walters as David Luiz (right) backs off
Arsenal inawezekana wamezipokea kwa shangwe habari za John Terry kusimamishwa mechi 4 na adhabu nyingine ya £220,000 baada  FA kumpata na makosa ya kumbagua Antoni Ferdinand. Olivier Giroud baada ya kusshusha presha baada ya kufunga goli la kwanza akiwa na jezi Arsenal kwenye michuano  ya kombe la ligi na inawezekana asifunge goli leo lakini uwepo wake mbele utawapa wakati mgumu Luiz na Cahili ktuokana na urefu na nguvu zake.

Vermaelen vs Koscielny vs Martesacker.
 Laurent Koscielny
Hakuna wakati mashabiki wa Arsenal na Arsene Wenger wana wakati mgumu  kama sasa ukiwaambia kati ya mabeki hawa nani aanze nani akae nje kwasababu wote wameonyesha sio tu kustahili kuanza kikosi cha kwanza lakini  pia  ni moja kati ya walinzi mahili kwa sasa ligi kuu ya Premier pale Uingereza.Msimu ulipoanza wengi walikuwa na uamuzi rahisi kumpa Vermaelen na Koscielny nafasi ya kuanza kutokana ubora waomsimu uliopita lakini kuumia kwa Koscielny kumempa nafasi Martesacker kuonyesha kwamba anastahili sio tu kuvaa jezi ya Arsenal lakini pia kuanza kikosi cha kwanza.

Vito Manone Vs Fernando Torres.
 Hot shot: Torres scores against Newcastle
Vito Manone anampa presha ya kutosha kipa namba moja wa Arsenal Wojciech Szcsezny kutokana uwezo ambao anaendelea kuonyesha.Anatakiwa kuendelea kumfanya mzee wenger aendelee kumuamini  hasa uikizingatia anakutana na safu ya ushambuliaji ya Fernando Torres  ambaye ameshaanza ule utaratibu wake wa kufumania nyavu. Vito Manone ni goli kipa mzuri na mashabiki wengi wa Arsenal wangependelea achukue nafasi hiyo moja kwa moja lakini binafsi naona aendelee kuwa msaidizi  mzuri wa Szcsezny kwani italeta ushindani ambao utakuwa na faida kwa Arsenal.

Sehemu ya kiungo.
 Playmaker: Eden Hazard
Sehemu ya kiungo ya Chelsea na Arsenal ndio kwa kiasi kikubwa itaamua mpambano huu kwani atakayeibuka kinara wa hili eneo kwa kiasi kikubwa ameshinda mechi hii.Kwa upande wa Chelsea John Obi Mikel atapewa jukumu alake la kawaida kutoa ulinzi kwa David Luiz na Gael Cahil na Frank Lampard,Oscar au Juan Matta atapewa nafasi ya kusambaza mipira na kutoa ubunifu katika eneo la hatari.Kwa upande wa Arsenal Mikel Arteta natakiwa kuendelea na anachokifnya kwa sasa kwani wengi hawamuongelei ila kwangu ni mtu mihimu sana kwani ndio analeta utulivu  muhimu katikati ya uwanja wakati Abou Diaby anatakiwa kuongeza pale alipoishia wiki iliyopita huku kama Arsenal wanachukua pointi tatu Emirates  leo basi Santiago Rodriguez Carzola analo jawabu.








0 comments:

Post a Comment