Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Sunday, September 23, 2012

NI VITA YA WANANCHI NA WANAJESHI



 All smiles: Joe Hart was furious in midweek following capitulation in Madrid - but his mood took a turn for the better at Carrington
 Kwa wale wapenzi wa soka jumapili hii ni sikukuu manake moto utawaka pale Etihad na pale kwenye uwanja wa Anfield.Hakika ni super Sunday ya Manchester City vs Arsenal na Liverpool vs Manchester United  kila shughuli itasimama kwa takribani masaa 3.Manake kama ni kula ule kabisa kabla ya saa 9 zaidi ya hapa unaweza usipate kabisa hamu ya kula manake ni hatari tupu kwa wale mashabiki wa timu hizi  ni patashika nguo kuchanika.Ila kwa hapa nitatatolea macho zadi mchezo baina ya the citizen au wananchi au Manchester City na washika bunduki wa London Arsenal pale katika dimba la Etihad hatari tupu.
Manchester City.

 Welcome back, Jack: Wilshere is closing in on a first-team return
 Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya premier pale Uingereza watapa nafasi ya kujiuliza wapi walikosea sio kwasababu walifungwa na Real Madrid lakini swali kubwa kwa Robert Mancini itakuwa kufungwa magoli mawili ndani ya dakika 5 pale Bernabeu.
Mashabiki wa Manchester City hawakufurahishwa kabisa na kiwango cha Joe Hart golini hasa akilaumiwa kwa goli la Cristiano Ronaldo.Robert Mancini baada ya mechi alimtetea Joe hart akisema wakulaumiwa ni yeye yani Mancini kwani ndio mwamuzi wa nani asimame golini
Lakini hakika kuelekea kwenye mchezo wa jumapili lazima ajitahidi kufuta makosa aliyoyafanya jumanne kama si hivyo atajikuta kwenye wakati mgumu sana kwani Arsenal japo Van Persie ameondoka  ila mechi dhidi ya Southampton imetuonyesha kwamba  bado wana watu wenye uwezo wa kufunga.
Manchester City watamkaribisha Sergio Kun Aguero baada ya kupona goti na kujumuishwa kwenye kikosi kilichocheza dhidi ya Real Madrid.Pablo Zabareta pia atarejea kikosini baada ya kupona maumivu ya nyama.Samir Nasri atakosekana kwa majuma kaza baada ya kupata majeraha kwenye mchezo dhidi ya Real Madrid pamoja na Mikah Richards naye ataendelea kukosekana kutokana na matatizo ya kifundo cha mguu.
UKWELI KUELEKEA MCHEZO WENYEWE.
Manchester City wameshafungwa magoli 6 mpaka sasa katika michezo 4 tu na kufikisha 20% ya magoli 29 waliyofungwa msimu uliopita.
Manchester City wamesharuhusu nyavu zao kutikiswa mara 13 kwenye michezo 7  katika mashindano yote waliyocheza.
Manchester City tangu wapoteze mchezo wao dhidi ya Arsenal mwezi wa nne msimu uliopita kwa 1-0 hawajapoteza michezo 10 mpaka sasa kwenye ligi kuu pale nchini Uingereza wakishinda 8 na kutoa sare michezo 2.
Manchester City hawajapoteza mchezo hata 1 katika michezo 31 ya ligi waliyocheza pale Etihad wakishinda 29 ni Fulham na Sunderland pekee ndio wamepata pointi hapa tangu mwezi wa Disemba mwaka 2010.

ARSENAL.
Arsenal kwa upande wao ilibidi wachimbe kweli kweli pale Estadio la Mosson kupata pointi tatu muhimu za kwanza katika UEFA Champions League.Olivier Giroud bado anatafuta goli lake la kwanza katika jezi ya Arsenal na kitu pekee ambacho mashabiki na wachambuzi wana imani nacho kwake anahitaji muda tu.Arsenal kwa sasa inaonekana kutengenezwa kumzunguka Santi Carzola na mara kazaa mwenyewe akisema eneo ambalo amepewa la kucheza huru kunamfanya ajisikie yuko nyumbani.
Kurudi kwa kiungo wa kutumainiwa Jack wilshere pamoja na Emanuel Frimpong ,Thomas Rosicky kunamfanya Wenger awe kocha mwenye wakati mgumu kuliko wakti wote pale Uingereza.Jack Wilshere amekosekana uwanjani kwa miezi 14 na kurudi kwake kunanifanya niione Arsenal bora kabisa kwa kipindi cha miezi 48 iliyopita.
UKWELI KUELEKEA MCHEZO.
Arsenal hawajafungwa michezo 9 katika mashindano yote wakishinda 4 na kutoa sare 5 na kipigo chao cha mwisho ilikuwa toka kwa Wigan mwezi wa April msimu uliopita.
Ushindi wa Arsenal wa hivi karibuni wa 6-1 dhidi ya Southampton ni ushindi wao mkubwa tangu waifunge Blackburn 7-1 mwezi February msimu uliopita.
Kama Andrei Arshavin akicheza mchezo wa jumapili utakuwa mchezo wake wa 100 wa ligi kuu nchini Uingereza.
Santi Carzola mpaka sasa ndio mchezaji ambaye ametengeneza nafasi nyingi za kufunga kwa wenzake kuliko mchezaji mwingine yoyote kwenye Premier ligi nchini Uingereza nafasi 14.
Mwamuzi wa mchezo wa jumapili ni Mike Dean na Arsenal wameshinda mchezo 1 tu katika michezo 14 ambayo Amechezesha.

WALIPOKUTANA.
Arsenal wameshindwa kufunga goli kwenye michezo 5 kati ya michezo 7 waliyokutana na Manchester City kwenye michuano yote.
Manchester City kwa upande wao wameshindwa kufunga goli hata moja kwenye michezo 4 kati ya 5 ya ligi ambayo wamecheza na Arsenal hivi karibuni.
Manchester City wameshinda michezo minne kati ya mitano ambayo wamecheza na Arsenal hivi karibuni katika michuano yote.
Katika kadi nne nyekundu zilizotoka kwenye michezo minne ya ligi kati ya Arsenal na Manchester  City kadi tatu zimeenda kwa Manchester City.
Katika mechi tatu za mwisho walipocheza msimu uliopita zote zimeisha kwa ushindi wa 1-0
Mabingwa watetezi Manchester City wameshinda michezo 29 na hawajapoteza hata mchezo mmoja katika michezo 30 waliyocheza pale Etihad.
Arsenal kwa upande wao wamepoteza mchezo 1 katika michezo 10 ya mwisho waliyocheza ugenini.
Tusubirie kipute cha dakika 90 pale Etihad Stadium
Hakika ni VITA YA WANANCHI NA WANAJESHI.

0 comments:

Post a Comment