Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Tuesday, August 21, 2012

POGBA AELEZA KILICHOMKIMBIZA MAN UTD

Paul Pogba

POGBA AELEZA KILICHOMKIMBIZA MAN UTD.
Mchezaji chipukizi wa zamani wa Manchester United Paul Pogba aliyejiunga na klabu ya Juventus ya nchini Italia msimu huu ameeleza sababu ya yeye kuondoka katika klabu ya Manchester United na kuhamia Juventus.Akizungumza na gazeti la L’Equipe Pogba mwenye umri wa miaka 19 anasema,”sijutii  uamuzi wangu wa kuondoka Man Utd analiambia gazeti la L’Eqipe.Nimejifunza mengi nikiwa na Man Utd lakini watu inabidi wanielewe na wauelewe uamuzi wangu.
Kocha Sir Alex Ferguson aliniamini sana lakini hakunipa nafasi ya kucheza na alikuwa akinieleza kuwa bado ni mdogo sana na hivyo niwe na subira kwani muda wangu wa kucheza utakuja ingawa haikuwa hivyo.Pamoja na kuwa alikuwa ni bosi wangu lakini ndoto yangu ilikuwa bado ni kucheza mpira kila mara katika kikosi cha Man Utd.
Nilipofika hapa Juventus,kocha Antonio Conte aliniambia wazi kuwa alikuwa anataka mchezaji wa kucheza pahala pa Pirlo pamoja na Vidal katika kikosi cha kwanza mana timu itashiriki michuano mingi na mikubwa hivyo anahitaji kuwa na mzunguko wa wachezaji katika idara ya kiungo.Pogba hakusita pia kuzungumzia kauli ya kocha wake wa zamani Ferguson yakuwa hakuwa na nidhamu kwa kusema’kauli ya kocha Ferguson ilinishangaza sana mana sikuwai kumkosea adabu Sir Alex ingawa kuna baadhi ya mambo tulishindwa kuelewana’.”



0 comments:

Post a Comment