Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Monday, August 13, 2012

BALOTELLI KUWAKOSA ENGLAND....


BALOTELLI KUWAKOSA ENGLAND...........
Mshambuliaji wa klabu ya Manchester City ya nchini England Super Mario Balotelli ameondolewa katika kikosi cha timu ya taifa ya Italia baada ya kugundulika kuwa na matatizo ya macho.Timu ya taifa ya Italia maarufu kama Azzuri itacheza mchezo wake wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya England siku ya tarehe 15 mwezi huu wa nane pale nchini Uswisi kama kalenda ya FIFA inavyosema.
Balotelli ambaye pia alishindwa kucheza katika pambano la Ngao ya Jamii siku ya Jumapli iliyopita dhidi ya Chelsea,atarudi uwanjani kama kawaida katika katika mechi za ligi kuu ya soka nchini England zinazotarajiwa kuanza mwishoni mwa juma hili.Katika kikosi cha Italia kilichotajwa na mwalimu Claudio Prandelli,wachezaji chipukizi wamepewa sana nafasi na zaidi ni klabu ya Atalanta kutoa wachezaji watatu katika kikosi hicho cha Azzuri.
Wachezaji hao ni pamoja na mshambuliaji Manolo Gabbiadini,beki Federico Peluso na golikipa Andrea Consigli.
Vikosi vya timu za zote ni hivi hapa
Kikosi cha Italia
Andrea Consigli (Atalanta), Mattia Perin (Genoa), Salvatore Sirigu (Paris St Germain); Ignazio Abate (AC Milan), Francesco Acerbi (AC Milan), Davide Astori (Cagliari), Federico Balzaretti (Roma), Mattia De Sciglio (AC Milan), Daniele Gastaldello (Sampdoria), Angelo Obinze Ogbonna (Torino), Federico Peluso (Atalanta); Alberto Aquilani (Fiorentina), Daniele De Rossi (Roma), Alessandro Diamanti (Bologna), Antonio Nocerino (AC Milan), Andrea Poli (Sampdoria), Ezequiel Schelotto (Atalanta), Marco Verratti (Paris Saint Germain); Mario Balotelli (Man City), Mattia Destro (Roma), Stephan El Shaarawy (AC Milan), Manolo Gabbiadini (Atalanta
Kikosi cha England
Magolikipa: Joe Hart (Manchester City), Jack Butland (Birmingham City), John Ruddy (Norwich City).
Mabeki: Leighton Baines (Everton), Ryan Bertrand (Chelsea), Gary Cahill (Chelsea), Steven Caulker (Tottenham Hotspur), Phil Jagielka (Everton), Kyle Walker (Tottenham Hotspur).
Viungo: Michael Carrick (Manchester United), Tom Cleverley (Manchester United), Frank Lampard (Chelsea), Adam Johnson (Manchester City), Jake Livermore (Tottenham Hotspur), James Milner (Manchester City), Alex Oxlade-Chamberlain (Arsenal), Jack Rodwell (Everton), Ashley Young (Manchester United).
Washambuliaji: Andy Carroll (Liverpool), Jermain Defoe (Tottenham Hotspur), Daniel Sturridge (Chelsea), Theo Walcott (Arsenal).

0 comments:

Post a Comment