Quintel Blogger theme

A free Premium Blogger theme from newbloggerthemes.com

Wednesday, August 15, 2012

BREAKING NEWS:MUAMBA AMUA KUSTAAFU SOKA.


Hatimaye Fabrice Muamba amemua  kuachana na soka baada ya ushauri kutoka kwa jopo la madaktari.Muamba alipata tatizo la moyo pale uwanja wa White Hat Lane kwenye mchezo wa kombe la FA baina ya timu yake ya Bolton Wonderes na Tottenham Hotspurs mwezi wa tatu. Moyo wa Muamba ulisimama kwa takribani dakika 78 kabla ya timu ya madaktari kufanya kazi ya ziiada pale uwanjani kabla ya kupelekwa Hospitali kwa matibabu zaidi.Baada ya kukaa nje kwa takribani mwezi mmoja hali ya Muamba ilikuwa inaendelea kuimarika siku hadi siku na kukawa na matumaini kwamba angeweza kurejea uwanjani hivi karibuni.
Wiki iliyopita Alisafiri kwenda Ubelgiji kukutana na daktari wa masuala ya moyo na akashauriwa kutokana na hali ya moyo wake hawezi kuendelea kucheza tena mpira.Kabla ya  kutangazwa rasmi kwa taarifa hiyo Muamba ailiandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kwamba”Watu waendelee Kutabasamu”.Muamba alifika England akitokea Kongo na kunza maisha yake ya soka na klabu ya Arsenal kabla ya kwenda Birmigham na baadae Bolton Wonderes.Muamba alicheza pia kwenye vikosi tofauti vya timu za Taifa za vijana Uingereza kabla ya haya maamuzi yake ya kustaaafu soka.

0 comments:

Post a Comment